Lissu ang’ang’ania video iletwe mahakamani, Katuga apinga hoja
Katuga: Kwenye ile video unachokiona ni nini, maneno au video?
Lissu: Sijaiona, si hamjaileta?
Katuga: Katika sheria ya ushahidi, mtu akikutolea ushahidi wa maneno, anatoa ushahidi wa kusikia?
Lissu: Ndiyo, wa kusikia kama ni wa maneno tu, ila kama ni video ni wa kuona na kusikia.
Katuga: Unatuhumiwa kufanya nini?
Lissu: Kutoa maneno na kuyachapisha.
Katuga: Umewaambia majaji kwamba upande wa Jamhuri haujathibitisha shtaka hilo kwa sababu video hawajaileta. Waambie mashahidi wa Jamhuri walisemaje.
Lissu: Walisema wameona video na kusikia maneno.
Katuga: Kwa hiyo waliona na kusikia?
Lissu: Huwezi kutenganisha video na sauti, kwa hiyo lazima iwe kuona na kusikia.
Katuga: Unajua kwamba kila shahidi ana haki ya kuaminiwa?
Lissu: Ndiyo, ninajua, na anastahili kuaminiwa kama kuna misingi ya kumuamini.
Katuga: Sasa iambie mahakama hii, katika mashahidi wa Jamhuri wale waliosema wameona video, ni kifungu kipi kinaelekeza kwamba lazima walete video hiyo mahakamani licha ya kwamba wameiona?
Lissu: Lazima wailete mahakamani ili waaminike.
Katuga: Iambie mahakama, ni kweli kwamba mtu anayepandisha video mtandaoni anaweza kuja kuifuta?
Lissu: Ndiyo.
Katuga: Unaelewa kwamba kitu fulani kinaweza kupotea ghafla. Kama mtu atakuwa amefanya kosa kwa kupandisha video yenye tatizo kisha akaifuta, iambie mahakama kwamba mtu huyo hawezi kuja mahakamani kutoa ushahidi? Kwa hiyo kilicholetwa hapa ni nini?
Lissu: Maneno na video havitengani. Video yenyewe haijaletwa.
Katuga: Tuiombe mahakama ikuchukulie wewe ni muongo?
Lissu: Jaji alisema hakumbuki, tuendelee.
Katuga: Unataka shahidi PW17, ambaye alisema alikusikia ukisema hayo maneno ya kukinukisha, ayalete hapa mahakamani?
Lissu: Ndiyo, ayalete hapa.
Katuga: Ni ushahidi wako kwamba mashahidi kutoka polisi waliandika maelezo yao wenyewe na kwa hiyo si wa kuaminika? Sasa mashahidi hawa wasiaminiwe kwa sababu wameandika maelezo wenyewe. Ni kifungu gani kinaipa mahakama mamlaka hayo?
Lissu: Kifungu cha 11 kinaelekeza kwamba polisi ambao hawakufuata utaratibu hawaaminiki.
Katuga: Wasomee majaji.
Lissu: (Anasoma.)
Katuga: Waambie majaji, kwa mujibu wa kifungu hicho, kimeeleza nini kuhusu polisi anayefanya upelelezi; anapaswa kuandika maelezo?
Lissu: Kama afisa huyo ni shahidi, basi haandikiwi maelezo.
Katuga: Afisa mdogo wa polisi anaweza kumwandikia afisa wa juu maelezo?
Lissu: Ndiyo, anaweza.
Katuga: Unajua kwamba maelezo ya shahidi yanaandikwa kwa mujibu wa sheria?
Lissu: Sikumbuki.
Katuga: Unajua kwamba tamko ni tamko la kiushahidi, na unajua kwamba shahidi lazima aonywe?
Soma Zaidi Hapa: