Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Kesi ya uhaini ya Tundu Lissu inaendelea leo

Lissu anaamini kuwa ameonewa, amesema ana chuki dhidi ya serikali sababu ya uonevu wake.

Muhtasari

Moja kwa moja

Elizabeth Kazibure, Rashid Abdallah & Asha Juma

  1. Lissu ang’ang’ania video iletwe mahakamani, Katuga apinga hoja

    Katuga: Kwenye ile video unachokiona ni nini, maneno au video?

    Lissu: Sijaiona, si hamjaileta?

    Katuga: Katika sheria ya ushahidi, mtu akikutolea ushahidi wa maneno, anatoa ushahidi wa kusikia?

    Lissu: Ndiyo, wa kusikia kama ni wa maneno tu, ila kama ni video ni wa kuona na kusikia.

    Katuga: Unatuhumiwa kufanya nini?

    Lissu: Kutoa maneno na kuyachapisha.

    Katuga: Umewaambia majaji kwamba upande wa Jamhuri haujathibitisha shtaka hilo kwa sababu video hawajaileta. Waambie mashahidi wa Jamhuri walisemaje.

    Lissu: Walisema wameona video na kusikia maneno.

    Katuga: Kwa hiyo waliona na kusikia?

    Lissu: Huwezi kutenganisha video na sauti, kwa hiyo lazima iwe kuona na kusikia.

    Katuga: Unajua kwamba kila shahidi ana haki ya kuaminiwa?

    Lissu: Ndiyo, ninajua, na anastahili kuaminiwa kama kuna misingi ya kumuamini.

    Katuga: Sasa iambie mahakama hii, katika mashahidi wa Jamhuri wale waliosema wameona video, ni kifungu kipi kinaelekeza kwamba lazima walete video hiyo mahakamani licha ya kwamba wameiona?

    Lissu: Lazima wailete mahakamani ili waaminike.

    Katuga: Iambie mahakama, ni kweli kwamba mtu anayepandisha video mtandaoni anaweza kuja kuifuta?

    Lissu: Ndiyo.

    Katuga: Unaelewa kwamba kitu fulani kinaweza kupotea ghafla. Kama mtu atakuwa amefanya kosa kwa kupandisha video yenye tatizo kisha akaifuta, iambie mahakama kwamba mtu huyo hawezi kuja mahakamani kutoa ushahidi? Kwa hiyo kilicholetwa hapa ni nini?

    Lissu: Maneno na video havitengani. Video yenyewe haijaletwa.

    Katuga: Tuiombe mahakama ikuchukulie wewe ni muongo?

    Lissu: Jaji alisema hakumbuki, tuendelee.

    Katuga: Unataka shahidi PW17, ambaye alisema alikusikia ukisema hayo maneno ya kukinukisha, ayalete hapa mahakamani?

    Lissu: Ndiyo, ayalete hapa.

    Katuga: Ni ushahidi wako kwamba mashahidi kutoka polisi waliandika maelezo yao wenyewe na kwa hiyo si wa kuaminika? Sasa mashahidi hawa wasiaminiwe kwa sababu wameandika maelezo wenyewe. Ni kifungu gani kinaipa mahakama mamlaka hayo?

    Lissu: Kifungu cha 11 kinaelekeza kwamba polisi ambao hawakufuata utaratibu hawaaminiki.

    Katuga: Wasomee majaji.

    Lissu: (Anasoma.)

    Katuga: Waambie majaji, kwa mujibu wa kifungu hicho, kimeeleza nini kuhusu polisi anayefanya upelelezi; anapaswa kuandika maelezo?

    Lissu: Kama afisa huyo ni shahidi, basi haandikiwi maelezo.

    Katuga: Afisa mdogo wa polisi anaweza kumwandikia afisa wa juu maelezo?

    Lissu: Ndiyo, anaweza.

    Katuga: Unajua kwamba maelezo ya shahidi yanaandikwa kwa mujibu wa sheria?

    Lissu: Sikumbuki.

    Katuga: Unajua kwamba tamko ni tamko la kiushahidi, na unajua kwamba shahidi lazima aonywe?

    Soma Zaidi Hapa:

  2. Lissu ajibu maswali kuhusu ushahidi wa video

    Katuga: Kama uliwaambia majaji hawa waendesha mashtaka hawajaleta video na kwamba, kwa kuwa mahakama haina video hiyo, wameshindwa kuthibitisha mashtaka yao, waambie majaji kama wakati unasema hayo ulikuwa unajua au umesoma mashtaka yanayokukabili.

    Lissu: Nilikuwa nimesoma mashtaka yanayonikabili na niliyaelewa kwa undani.

    Katuga: Kwa mujibu wa mashtaka, kuna sehemu unashtakiwa kwa kuchapisha video?

    Lissu: Nashtakiwa kwa kuchapisha maneno kwenye mtandao wa Jambo TV.

    Katuga: Je, nitakuwa sahihi nikisema video unasikia na kuona kama video hiyo ina maneno?

    Lissu: Video ni kuona na kusikia. Kwa mujibu wa sheria ya ushahidi, mtu akitoa ushahidi kuhusiana na maneno anakuwa ametoa ushahidi wa kusikia.

    Katuga: Kwa mujibu wa mashtaka, unatuhumiwa kuyachapisha na kutoa maneno kwenye mtandao wa YouTube wa Jambo TV. Uliiambia mahakama kuwa upande wa Jamhuri haujathibitisha mashtaka kwa sababu video hiyo hawajaileta?

    Lissu: Mashahidi wote wa Jamhuri walisema kuwa wameona na kusikia maneno.

    Katuga: Unafahamu kwamba kila shahidi ana haki ya kuaminiwa isipokuwa kama mahakama ina sababu za kutomuamini, na sababu hizo lazima zionyeshwe? Iambie mahakama hii, wale mashahidi waliosema wameona video, ni kifungu gani cha sheria kinachosema kuwa ili waaminiwe lazima walete video?

    Lissu: Si lazima sheria iseme hivyo, bali hiyo ni common sense.

    Katuga: Ni kweli kwamba mtu anayeipandisha video mtandaoni ana uwezo wa kuifuta?

    Lissu: Ana uwezo huo.

    Katuga: Je, mtu akiwa amefanya kosa kwa kuchapisha video mtandaoni halafu akaifuta, na mtu mwingine akaiona video hiyo kabla haijafutwa, ni ushahidi wako kwamba hawezi kuthibitisha alichoona?

    Lissu: Hawezi kuthibitisha.

    Katuga: Video na maneno, kilicholetwa hapa mahakamani ni nini?

    Lissu: Wameleta maneno tu, na hayo si maneno ya kwenye video, kwa sababu maneno ya video huwezi kuyatenganisha na video yenyewe.

    Katuga: Unakumbuka PW17 ndiye shahidi pekee aliyekuwa live eneo la tukio?

    Lissu: Ndiyo.

    Katuga: Unakumbuka shahidi PW17 alisema Lissu alisema atauzuia uchaguzi?

    Lissu: Sikumbuki.

    Katuga: Kwa kuwa shahidi alikuwa eneo hilo, alihitajika kuileta video hiyo?

    Lissu: Alipaswa kuileta video hiyo.

    Katuga: Anasema alikusikia ukisema unaenda kuzuia uchaguzi na kwamba utaenda kukinukisha. Je, unataka shahidi huyo alete video hapa mahakamani?

    Lissu: Ndiyo, lazima.

    Katuga: Ni ushahidi wako kwamba mashahidi kutoka Jeshi la Polisi hawaaminiki kwa sababu waliandika maelezo bila kufuata utaratibu?

    Lissu: Ni kweli hawaaminiki kwa sababu hawakufuata utaratibu.

    Katuga: Ni kweli kwamba mashahidi wote uliowataja walikuja hapa mahakamani kutoa ushahidi, na kwa kufanya hivyo mahakama imepata fursa ya kutathmini uaminifu (credibility) wao?

    Lissu: Hayo ni ya majaji.

    Katuga: Ni kifungu gani cha sheria kinachoipa mahakama mamlaka ya kutowaamini polisi waliokuja kutoa ushahidi?

    Lissu: Utaratibu wa kuandika maelezo upo chini ya Kifungu cha 11(4) cha CPA. Kifungu hicho hakijaeleza chochote kuhusu hilo.

    Katuga: Umesema maelezo haya yalitakiwa yaandikwe mbele ya afisa wa polisi na si mpelelezi.

    Lissu: Ndiyo.

    Unaweza kusoma;

  3. Lissu akiri kuridhia yaliyomo kwenye vielelezo vyake mahakamani

    Katuga: Unakumbuka kwamba uliambia mahakama kuwa umetoa vielelezo D1 hadi D15. Je, ni vielelezo vyako au si vyako?

    Lissu: Ni vyangu kwa sababu mimi ndiye niliyeomba viingizwe mahakamani.

    Katuga: Je, nikisema kwamba uliomba vipokelewe mahakamani kama vielelezo vyako, umeridhika na yaliyomo ndani ya vielelezo hivyo?

    Lissu: Ndiyo, nimeridhika.

    Katuga: Umeridhika vitumike kama vielelezo vyako, na unaridhika na vielelezo ulivyovitoa?

    Lissu: Nimeridhika vitumike katika utetezi wangu.

    Katuga: Waheshimiwa Majaji, tunaomba vielelezo D1 hadi D15 ...

    Soma Zaidi Hapa:

  4. Uko timamu mzee wangu? Lissu aulizwa na upande wa serikali

    Katuga: Naona tutakaa hapa siku mbili

    Lissu: Unanitisha na siku mbili nimekaa ndani mwaka na miezi mitano

    Katuga: Iambie mahakama ulinzi wa mashahidi maana yake nini

    Lissu: Ni mashahidi wa kificho/ ni mashahidi wanaolindwa

    Katuga: Iambie mahakama, Je, ulisema baadhi ya watu huenda tulikuwa nao humu ndani. Je, huu ni ushahidi au hisia tupu?

    Lissu: Ndio ni shahidi wangu sababu hawajulikani hakuna anayewajua isipokua nyie

    Katuga: Je ushahidi wa kwamba hawa ni mapolisi. Je, ni ushahidi au fununu tu?

    Lissu: Ni ushahidi sababu hawajulikani na yeyote

    Katuga: Sasa shahidi tunataka majibu sahihi ni kweli au sio kweli. Ushahidi wa kwamba baadhi ya mashahdi huenda tulikuwa nao humu ndani. JE, ni kweli, sio kweli, sio wa kuona wala kusikia?

    Lissu: Sio Kweli

    Katuga: Iambie mahakama kama ni kweli au sio kweli unatuhuma nyingie za kuchapisha uongo mtandaoni

    Lissu: Ni kweli

    Katuga: Iambie mahakama unakumbuka ulisomewa hoja za awali na ikaanza kusikilizwa

    Lissu: Ndio nianakumbuka

    Katuga: Unakumbuka uliposomewa hoja za wali ulisema majaji ni ma-CCM

    Lissu: Sikumbuki

    Katuga: Iambie mahakama hii katika hotuba yako pia ulitangaza kutogumbea kwa chama chako

    Lissu: Sikumbuki, nakumbuka nilisema tutahamasisha ….

    Katuga: Hapana, hukumbuki nimsekia ukijiita mwenyekiti wa Chadema. Iambie mahakama kama chama chako kilishiriki uchaguzi mwaka jana

    Lissu: Hapana hakikushiriki

    Katuga: Je, ni kweli kwamba uliposema mahakamani hakuendeki huna imani na mahakama

    Lissu: Kwenye maswala haya ya uchaguzi sina imani na mahakama

    Katuga: Kwenye zile njia ulizotuambia jana. Je, nitakuwa sahihi kwamba hukupanga kabisa kuiomba mahakama kutumia sheria

    Lissu: Sikupanga kabisa

    Katuga: Kwa hiyo ni sahihi kwamba swala la kupinga sheria kwa njia ya mahakama sio njia mbadala wala ya kidemokrasia

    Lissu: Hapana

    Katuga: Kwa hiyo kukinukisha ni njia ya kidemokrasia?

    Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

    Katuga: Kuhamasisha uasi ni njia ya kidemokrasia?

    Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

    Katuga: Uko Timamu mzee wangu

    Lissu: Kimya

    Katuga: Kama nilikusia ulitamka vifungu vya 55, 63, 52 kifungu cha 52 cha sheria ya habari. Ni kweli kwamba sheria ya habari iliundwa kwa ajili ya kuendesha tasnia ya habari?

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kama nilikusikia vyema ulisema kuikosoa serikali sio kosa

    Lissu: Nilisema kuipinga serikali sio kosa

    Katuga: Kama una kanuni yako ya adhabu hapo kwa ridhaa ya mahakama hiki kifungu cha 55, yale maneno uliyotumbua, 'ya kuzuia uchaguzi' waambie majaji kuzuia uchaguzi ni kuipinga serikali au kuzuia uchaguzi?

    Lissu: NI kuzuia uchaguzi

    Katuga: Kuhamasisha uasi, kukinukisha nikupinga serikali au kupanga kuipindua serikali?

    Lissu: Ni kuipinga serikali, sikuwa nazungumza habari ya serikali tulikuwa tunapanga kuzuia uchaguzi

    Katuga: Unakumbuka umesema kwenye hotuba yako ulikuwa huzungumzii serikali

    Lissu: Ndio sikuwa napinga serikali nilikua nazungumza habari za uchaguzi

    Katuga: Kama nikikusikia vyema uliwaambia waheshimiwa hawa mashahidi wanaotoka jeshi la polisi, kasoro mmoja, wote wamejiandikia maelezo kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Waambie majaji kama uliwatajia kifungu cha sheria na sheria yenyewe

    Lissu: Sikuwaambia kifungu lakini kipo

    Katuga: Unajua kwamba askari aliyemuandika shahidi maelezo na yeye ni shahidi kama huyo shahdi hata fika mahakani

    Lissu: Sikumbuki

    Soma Zaidi Hapa:

  5. Lissu aendelea kujibu maswali ya upande wa serikali

    Katuga: Kama nilikusikia vyema uliiambia mahakama hii kwamba shahidi PW1 hakusema kama alivyogundua ni kosa la uhaini hakuwasiliana na ngazi za juu akiwemo DCI, kwamba ilipelelezwa vibaya

    Lissu: nilisema ilipelelezwa vibaya

    Katuga: Iambie mahakama kama sheria inaelekeza ukigundua kosa la uhaini lazima uwasiliane na hizo mamlaka zote, imabie mahakama kama ulitaja kifungu

    Lissu: Hapana sikutaja kifungu

    Katuga: Je unakumbuka ulisema kuna kutoelewana kati yako na Kingai (Kamishna wa Polisi Ramadhani Kingai ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini Tanzania) pamoja na IGP Wambura (Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Camillius Wambura)

    Lissu: Ni kweli nimekamatwa mara kadhaa bila kuzingatia taratibu

    Katuga: Umekuwa mwanasheria muda mrefu na mwana siasa miaka 24. Je, ushawafunguliwa wawili hawa mashitaka?

    Hapana: Sijawafungulia

    Katuga: Kama nimekusikia vizuri uliambia mahakama hii kwamba wale mashahdi walioletwa ni mashahidi ambao walikuwa ni washitakiwa

    Lissu: Nilisema walikiri kupanga uhalifu

    Katuga: Je, kuna sheria inayozuia mtu aliyefanya uhalifu kuja kutoa ushahidi?

    Lissu: Hapana

    Katuga: Katika ushahidi wa mashahidi toka Jeshi la polisi walieleza walikamata wote

    Lissu: Waliokamata waliweza kuwatambua

    Katuga: Kwa ushahidi huo ina maana inawezekana kukawa na wengine

    Lissu: Hawakutambuliwa au hawakukamatwa

    Katuga: Nakukumbusha ile kauli yako si ndio uliambia mahakama mtu yeyote anaweza kutafsiri vyovyote vile na wale walisema wamehamasika kutokana na nini

    Lissu: Maneno yangu

    Katuga: Kwa hiyo nitakuwa sahihi nikisema walielewa hotuba yako na kufanyia kazi maneno yako kwa jinsi walivyoelewa

    Lissu: Hapana siwezi sema sababu siwajui na siwezi kuwasemea

    Katuga: Je, uliiambia mahakama hawa mashahidi ni waongo na hawastahili kuaminiwa na mahakama?

    Lissu: Ndio, niliambia mahakama hawapaswi kuaminiwa wao na ushahidi wao

    Soma Zaidi Hapa:

  6. Upande wa serikali unaendelea na maswali ya dodoso kwa Tundu Lissu

    Wakili wa serikali (Nassoro Katuga): Umesema umepata tuzo kadhaa kwa kupigania haki. Je, ulitaja nchi za Afrika ulizopigania haki?

    Lissu: Hapana

    Katuga: Je uliiambia mahakama pamoja na kukaa kwako gerezani unasema heshima yako imeongezeka. Waambie majaji ni lini ulifanya huo utafiti ukajua heshima yako imeongezeka?

    Lissu; Heshima haitokani na sensa

    Katuga: Sasa wewe umejuaje heshima yako imeongezeka?

    Lissu: Heshima inaongezeka kwa watu kukuheshimu

    Katuga: Oooh pamoja na wazungu?

    Lissu: Hapana, sio wao tu, watu wote zikiwemo taasisi za kimataifa

    Katuga: Shahidi kama nilikuelewa vyema ukiwa unazungumzia mapungufu ya sheria za uchaguzi ulimuelezea mgombea wako wa jimbo la Mlimba kwamba alirudisha fomu akamkuta mtu hayupo. Ulikuwepo au uliambiwa?

    Lissu: Niliambiwa na nilisoma kweye taarifa rasmi

    Katuga: Waambie majaji kuwa mashahidi wa Jeshi la Polisi, hao mashahidi wa kificho hawajulikani na mtu mwingine

    Lissu: Ndio

    Katuga: Waambie waheshimiwa majaji kama uliwahi leta pingamizi juu ya kizimba cha mashahidi wa siri

    Lissu: Ndio

    Katuga: Iambie mahakama maamuzi ya mahakama ni nini

    Lissu" Waliamua wawaone wao

    Katuga" iambie mahakama hawa ulikua unawaIta P ni akina nani

    Lissu: Hayo ni majina, hizo ni alama, hayo ni mambo ya kuwaficha

    Katuga: Je unajua maamuzi ya mahakama hii juu ya kuficha utambulisho wa mashahidi

    Lissu: Iliamua wafichwe

    Katuga: Imabie mahakama ni sheria gani inayotaka ujue jina la shahidi ndio shahidi atoe ushahidi

    Lissu: CPA na Sheria ya Ushahidi inaelekeza mpaka ajulikane

    Katuga: Iambie mahakama

    Lissu: Kwa CPA na sheria ya mwenendo wa ushahidi, lazima afahamike na majaji na mahakama na watuhumiwa na sio upande wa utetezi peke yake

    Katuga: Waambie majaji ni kifungu gani cha CPA

    Lissu: Naomba nisome waheshimiwa majaji ni kifungu cha 112 kinachosema mashahidi watatoa ushahidi mbele ya hadhara ya mahakama na utambulisho wao utawekwa wazi, majina, dini zao na makazi yao

    Katuga: Je, kifungu kinasema hawatatoa ushahidi mpaka majina yao ya kweli yafhamike

    Lissu: Ndio hivyo kifungu kinasema

    Katuga: Waambie majaji wapi pameandikwa majina ya kweli yatajwe

    Lissu: Hakuna ila ni lazima mahakamma itambue utambulisho wao

    Katuga: Hivi unakumbuka wakati PW17 aliiambia mahakama baada ya kutoa hotuba, mliwatoa nje waandishi ili mkae kikao cha ndani

    Lissu: Ndio

    Katuga: Waambie majaji kama uliwahi kukanusha kama mliwatoa waandishi nje

    Lissu: Ndio hayakuwa yanawahusu tuliwaita kwa ajili ya mkutano na watia nia na sio zaidi ya hapo na baada ya kuwatoa waliondoka sio kwamba tuliwatoa na kuwarudisha

    Katuga: Unajua majibu yako yanavutia sana

    Lissu: Inabidi ufurahi kama yanavutia

    Katuga: Kwa hiyo nicheke cheke

    Lissu: Ndio cheka cheka si yanavutia sasa

    Katuga: Tafsiri sahihi inamaana wewe na wenzako mliwatoa waandishi wa habari

    Lissu: Ndio tuliwatoa

    Katuga: Mnasema mliwatoa sababu hayakua sehemu ya yale mliyowaitia

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kwa hiyo yale ambayo hamkutaka yachapishwe mliwatoa nje

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kwahiyo unawaambia majaji yale yaliyochapishwa ni yale uliyotaka yachapishwe

    Lissu: Ndio yote tuliyotaka wawepo walikuepo waandishi wa habari na si vinginevyo, ila sikuwa lazimisha wachapishe

    Soma Zaidi Hapa:

  7. Habari picha: Matukio ya kabla ya kuanza kwa kesi ya Tundu Lissu

  8. Kesi ya uhaini ya Tundu Lissu kuendelea leo

    Kesi ya uhaini inayomkabili mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inaendelea tena leo katika mahakama jijini Dar es Salaam, baada ya kuahirishwa hapo jana.

    Mwenendo wa kesi hapo jana ulifikia katika hatua ya upande wa serikali kumuuliza mshtakiwa maswali ya dodoso baada ya Lissu kuwasilisha ushahidi wa kujitetea.

    Soma Zaidi Hapa:

  9. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya kesi ya uhaini ya Tundu Lissu, tarehe 27/08/2026

  10. Maswali ya dodoso kwa Lissu yakiendelea

    Katuga: Kama nimekusikia vyema umesema ulitoa hotuba kwa watia nia wa Chadema na pia ulitoa hotuba hii mbele ya waandishi wa habari waambie majaji kama katika ushahdi wako umewaambia waandishi wa habaari wasipeleke rekodi zile na yale mliyozungumza.

    Lissu: Hapana sikuwaambia.

    Katuga: kwa hiyo ulitaka habari yako iende kwa walaji?

    Lissu: Ndio nilitaka iwafikie wananchi.

    Katuga: Katika ushahidi wako ulisema kama ulitoa mipaka kwa watu wanaopaswa kusikia ile hotuba.

    Lissu: Hapana sikutoa mipaka

    Katuga: Wale watia nia ulikua nao pale ambao ndio ulikuwa umewakusudia?

    Lissu: Ndio walikuwepo

    Katuga: Waambie majaji kama unakumbuka mkutano ulikuwa mubashara.

    Lissu: Ndio ni kweli

    Katuga: Waambie majaji kama uliwapa waandishi wa habari hotuba yako kabla kuzungumza.

    Lissu: Hapana sikuwapa.

    Katuga: Hivyo walikuwa hawajui unakwenda kuzungumza nini?

    Lissu: Ni sahihi

    Katuga: Kwa kuwa walikuwa hawajui nitakuwa sahihi nikisema haya maneno PW17 na wenzake walikuwa hawajui kabla ya wewe kuyatamka.

    Lissu: Ndio walikuwa hawajui.

    Katuga: Unakumbuka mashahidi walisema ulikuwa umevaa kombat na tishrt nyeusi?

    Lissu: Ndio nakumbuka.

    Katuga:Kuna sehemu umekanusha vazi ulilokuwa umevaa.

    Lissu: Ningekanushaje vazi langu rasmi la chama?

    Katuga: Kwa kuwa unasema ilikuwa hivyo nitasema mashahidi wa jamuhuri walikutambua kwa usahihi baada ya kutazama ile video.

    Lissu: Ninasema mashahdi wa jamhuri wananitambua siku nyingi ni sahihi nilikua nimevaa hivyo.

    Katuga: Unajua Principle ya constructive possession na constrtuction

    Lissu: Hapana siijui.

    Katuga: Umeiambia mahakama unakumbuka PW 17 alisema alichapisha kupitia wewe?

    Lissu: Hapana alisema walichapisha wao kupitia Mimi. Waheshimiwa majaji naomba nikae hii mvua ya maswali inanielemea.

    Jaji: Kaa.

    Katuga: Unapotoa hotuba kila mtu si ana haki ya kuelewa na kutelekeza vile alivyoelewa?

    Lissu: Ndio ni kweli

    Katuga: Maneno ya kwamba tutazuia uchaguzi si kila mtu ana haki ya kuelewa alivyolewa?

    Lissu: Ndio Maneno kama Tutazuia uchaguzi si kila mtu ana haki ya kuzuia uchaguzi kwa kutumia njia yake mwenyewe

    Katuga: Unakumbuka PW3 alipotoa ushahidi na kusema walipanga kuzuia uchaguzi kwa kurusha mawe kuchoma moto baada ya kauli zako walipanga kurushia watu mawe wasiende kupiga kura iambie mahakama hii kwamba uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria.

    Lissu: Ndio

    Katuga: Mojawapo ya kazi za serikali ni kusimamia sheria

    Lissu: Ndio

    Katuga: Je, kuzuia watu kwenda kupiga kura kwa kuwarushia mawe ni uvunjifu wa amani sio ubunjifu wa amani?

    Lissu: Ndio ni uvunjifu wa amani

    Katuga: Na Jeshi la polisi liko chini ya nani?

    Lissu: Jeshi la Polisi liko chini ya serikali

    Katuga Unapotishia kuvunja amani umemlenga nani?

    Lissu: Hapana unapovunja amani hujalenga polisi.

    Katuga: Utanijibu tu ujanja hauna.

    Lissu: Twende

    Katuga: Anapotishia kuvunja amani anakuwa amefanyaje?

    Lissu: Anakuwa analipa Jeshi la polisi kazi ya kumzuia asivunje amani.

    Katuga: Kama niko sahihi ulisema unataka kuhamasisha maandamano ya kidemokrasia, je, kwenye haya maneno kuna maneno utahamasisha uasi wa kidemokrasia?

    Lissu: Hapana

    Katuga : Je, video ililetwa mahakamani au haikuletwa wewe si mkweli?

    Lissu: Ililetwa ikakataliwa na mahakama.

    Katuga: Je, wewe ungependa kuiona na kuiomba mahakama hii tukufu iilete mahakamani?

    Lissu: Hapana hamuwezi mkaleta takataka nije niwasaidie mimi.

    Katuga: Demokrasia inatoa haki kwa wote waounga mkono na wasio unga mkono yule anapenda kupiga kura. Je, yale maneno kuzuia uchaguzi yanatokana na demokrasia gani?

    Lissu: Kama kuna jambo mnaona halipendezi mna haki ya kukipinga na kuliondoa kwa mujibu wa sheria.

    Katuga: Je, unajua kuzuia uchaguzi ni kosa?

    Lissu: Hapana sheria haijasema.

    Katuga: Je, bado unasisitiza katiba inasema ni haki ya kikatiba kumzuia mtu kupiga kupiga kura kwa kufanya fujo?

    Lissu: Katiba sio ibara moja.

    Katuga: Tafsiri ya adhabu inaposema shall be liable pale ambapo kifungu cha sheria kinatoa maneno shall be liable je, kuna descretion ya mahakama?

    Lissu: Hapana.

    Katuga: Uko aware na kesi ya Shengi Muhagama?

    Lissu: Niko Gerezani nitajuaje?

    Katuga: Si ulikua unatoa kesi hapa?

    Lissu: Wewe unaangalia mtandaoni hapo mimi naanngalia wapi?

    Katuga: Si una watafiti we mzee?

    Lissu: Waambie mmenishtaki kunyongwa kosa la bure.

    Katuga: Unaweza kuisaidia mahakama tofauti ya mkanganyo na hapa halipo.

    Lissu: Mkanganyiko ni kama jambo linalokuwa na maelezo mawili yanayotofautiana lakini omission ni jambo ambalo halipo lakini limechomekewa.

    Katuga: umewahi kufungua shauri kwa jina lako kupinga sheria ya uchaguzi?

    Lissu: Hapana, kwa chama changu Yes

    Katuga: Kama nilikusikia vyema umeleta mambo ya jaji chande sana ya 29/10

    Lissu: Ndio

    Katuga: Je ni kweli kwamba ripoti yake ilisema pia matukio haya yalipangwa kabla kutokana na malalamiko ya muda mrefu ya mifumo ya uchaguzi, katiba ajira ……

    Lissu: Nisomeee unikumbushe.

    Katuga: Kwenye hotuba yako tuambie kama ulisema tukikinukisha watatufanya nini?

    Lissu: Hapana.

    Katuga: Sasa ulisema watanikamata watanifungulia kesi ya uhaini?

    Lissu: Hapana.

    Katuga: Unakumbuka kuwaambia majaji ni ma CCM?

    Lissu :Ndio.

    Katuga: Waheshimiwa majaji bado tuko nusu ila nikiangalia muda naona ni saa 11

    Jaji: Mshtakiwa unasemaje?

    Lissu: Waheshimiwa majaji kama ni saa 11 inatosha nimesimama ya kutosha kwa leo.

    Jaji: Kimsingi tunatamani kuanza saa tatu kamili ili tuwe tumetumia muda vyema. Tutakapowahi tutaanza.

    Tunahirisha mpaka kesho saa tatu asubuhi.

  11. Lissu: Nina chuki dhidi ya serikali sababu ya uonevu wake

    Katuga: Nimekusikia umesema vitu vingi sana kuhusiana na CV yako pamoja na matatizo yaliyokukuta wewe unayaita mapambano sasa hivyo vitu vyote iambie mahakama wewe ni mtu mwenye chuki dhidi ya serikali

    Lissu: Ndio nina chuki dhidi ya watu kuonewa

    Katuga: Unaamini umeonewa na una chuki na mahakama i note unachuki.

    Lissu: Ndio nina chuki dhidi ya serikali sababu ya uonevu wake.

    Katuga: Kama mwanasiasa nia ya chama cha siasa ni kushika Dola.

    Lissu: Ndio kushika dola ni moja wapo.

    Katuga: Iambie mahakama hii kama unafahamu mihimili mitatu ya dola.

    Lissu: Ndio ninaifahamu ni serikali, mahakama na bunge

    Katuga: Uko kwenye nafasi nzuri sana ya kunipa elimu, kwenye swali la kisheria hii mihimili mitatu kazi yake ni nini?

    Lissu: Bunge kazi yake ni kutunga sheria

    Katuga: Kazi ya mahakama ni nini?

    Lissu: Ni kutafsiri sheria na inatengua sheria na ikitengua maana yake bunge limetunga sheria ya hovyo.

    Katuga: Kazi ya serikali baada ya sheria kutungwa ni nini?

    Lissu: Kuzilinda sheria.

    Katuga: Mtu akitengeneza nia ya kutishia serikali tafsiri kama mwanasheria kuna takwa kisheria kwamba lazima hiyo serikali lazima iwe imetishika.

    Lissu: Hakuna hiyo provision lakini.

    Katuga: Hapana swali langu ushajibu.

    Lissu: Nataka kuisaidia mahakama, kwenye sheria bado inaeleza lazima kuwe na matokeo.

    Katuga: Leo tutakesha

    Lissu: Nimekaa mwaka na miezi mitano unaogopa kukesha?

    Katuga: Umesema baadhi ya mashidi ni mapolisi walioko kwenye jeshi linaloendeshwa na IGP wambura na DCI Kingai iambie mahakama ulikuepo au umesikia au ilikuwaje?

    Lissu: Ndio ni mapolisi wanaotumia jeshi linaloongozwa na wambura na Kingai ambao wamenipersecute kwa muda mrefu na nilisema hivyo sababu ya maandishi ya mashahidi hao.

    Katuga: Ni kweli umewataja watu hawa waje kukutetea mahakamani?

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kwa hiyo ni mashahidi wema

    Lissu: Hapana sio wema nitakuja kuwauliza waeleze jinsi wanavyoelewa kesi hii

    Katuga: Lissu ulikamatwa au ulichukuliwa?

    Lissu: Nilikamatwa kama hujawahi kamatwa huwezi kuelewa

    Katuga: Unajuaje kama sijakamatwa

    Lissu: Nyie mnawekelea watu maneno mnakamatwa namna gani?

    Katuga: Kama nimekusikia vyema embu iambie mahakama dhumuni la kuwa na hoja za awali preliminary hearing.

    Lissu: Lengo lake ni kuchambua na kuweka kando vitu ambavyo vinabishaniwa.

    Katuga: Unajua yale mambo ambayo hayaihitaji kubishaniwa hayahitaji mashahidi na ulikubali hayana ubishani?

    Lissu: Ndio

    Katuga: Wakati unaeleza majaji mashahidi wawili walikuwa Mbinga wakati wa ukamataji ulitaka waje wafanye nini?

    Lissu: Ndio nilitaka waje waieleze mahakama kila kitu, nilikamatwa kweli lakini uhalali wa ukamataji hilo ni suala jingine.

  12. Lisu aendelea kujibu maswali ya dodoso

    Katuga: Kaka yetu wewe msomi sana historia ulisoma pia?

    Lissu: Ndio nimesoma historia

    Katuga: Kuna wakoloni waliingia mkataba ya kilaghai na baadhi ya viongozi ili waweze kutawala baadhi ya maeneo

    Lissu: Hapana ilikuwa mikataba ya kuwanufaisha viongozi wenyewe waaliingia mikataba na machifu, machifu ndio akina Samia wa sasa hivi.

    Katuga: Unataka tukae sana huko.

    Lissu: Twende kaka

    Katuga: Isaidie mahakama, kama unakumbuka awamu ya tano ilizuia makinikia kutoka na wewe ukatetea makinikia yatoke sababu wazungu watatudai mapesa mengi.

    Lissu: Hapana sikusema hivyo nilieleza hasara ya kufanya hivyo unataka nikueleze mashtaka ya Tanzania huko duniani?, huko usiende

    Katuga: Tuendeleee leo niko na wewe, unakumbuka wewe ulisema ulikuwa Rais wa TLS iambie mahakama wakati unashtakiwa ulikuwa Rais wa TLS?

    Lissu: Hapana

    Katuga: Kama nilikusikia vyema unasema wewe ni mwaminifu umeongoza vita vya kupigania haki za binadamu na rasilimali na ulipigana vipi hii vita?

    Lissu: Ndio nilieleza kazi nilizofanya kupigania rasilimali za nchi hii.

    Katuga: Kama nilikusikia vizuri ulisema wewe ni mtaalamu sana wa sheria za uchaguzi na wewe ni mtaalamu wa sheria.

    Lissu: Ndio

    Katuga: Tanzania kupinga sheria fulani inayokinzana na katiba utaratibu uko vipi?

    Lissu: Kuna njia nyingi unaweza kuleta petition, kuhamasisha wanachi kufanya maandamano kupinga sheria husika na moja wapo hii ya kuja mahakamani.

    Katuga: Kifungu cha nne

    Lissu: Ndio au kama unaanzia mahakama ya chini kifungu cha tisa

    Katuga: Iambie mahakama na hiyo ya kupinga sheria kwa maandamano iko kwa kifungu gani

    Lissu: Iko kwa kifungu cha 20:1 inayoruhusu watu kufanya mijumuiko kidemokrasia maandamano ya kidemokrasia yanaruhusiwa kikatiba na kisheria unatumia vyombo vya habari na yote haya ni njia za kubadilisha sheria.

    Katuga: Waheshimiwa majaji tunaomba atusomee

    Lissu anasoma, kila mtu ana haki ya kukutana na watu wangine kwa amani na kutoa maoni yake kwa uhuru na amani.

    Katuga: Hicho ulichoelewa

    Lissu: Ndio, ndio ushahidi wangu

    Katuga: Unamjua mtu anaitwa Francis Ndyanabo

    Lissu: Julius Francis Ishengoma Ndyanabo, wakili mwenzangu alifungua shauri kupinga sheria ya uchaguzi.

    Katuga: Alishinda, alishindwa?

    Lissu: Alishinda

    Katuga: Na Mtikila unamfahamu?

    Lissu: Kuhusu mgombea binafsi Mchungaji Christopher Mtikila alishinda hapa ndani na mahakama ya Afrika na serikali unayoitumikia imekataa kutekeleza uamuzi huo mpaka leo.

    Katuga: Umemtaja sana Rugemeleza Nshala iambie mahakama hii kama Nshala ni shahidi wako.

    Lissu: Hapana ni wakili mwenzangu yuko hapa na alikuwa mshitakiwa mwenzangu.

    Katuga: Kuna njia ngapi za kudhurisha nia

    Lissu: Publication, or oral

    Katuga: Iambie mahakama linapotumika neno or yanatumika kwa pamoja au vipi?

    Lissu: Hapana ila yanaweza kufana au yasifanane na kiswahili chake ni kitendo

  13. Upande wa jamhuri unamuuliza maswali mshtakiwa

    Baada ya mlo wa mchana, upande wa jamuhuri wako tayari kwa ajili ya maswali ya dodoso kwa mshtakiwa.

    Nassoro Katuga: Shahidi pole na ushahidi mrefu

    Lissu: Ahsante sana

    Katuga: Kama nimekusikia vyema ulisema utatuacha sisi ndugu zako tukuulize maswali.

    Lissu: Sahihi.

    Katuga: Waambie majaji hiki tunachokifanya ni kitu cha kisheria na hakina nasaba nyingine yeyote.

    Katuga: Uliiambia mahakama wewe ni wakili wa mahakama kuu na una ujuzi wa kisheria.

    Lissu: Ndio

    Katuga: Hebu waambie majaji Tanzania ilipata uhuru mwaka gani.

    Lissu: 9/12/1961

    Katuga: Kwa majibu hayo Tanzania ni nchi huru.

    Lissu: Ndio

    Katuga: Chombo cha mwisho cha kufanya maamuzi ya mwisho kwa mujibu wa kisheria ni ni kipi?

    Lissu: Mahakama

    Katuga: Mahakama haitakiwi kuingiliwa na mtu yeyote inapotoa maamuzi na pia mahakama hailazimishwi wala haipingwi na mtu au chombo chochote toka nje au ndani.

    Lissu: Sahihi haipangiwi walakulazimishwa.

    Katuga: Umetuambia wewe ni Mwenyekiti wa Chadema, Je katika utetezi wako umeimbia mahakama hii kuwa mwenyekiti wa Chadema ana kinga?

    Lissu; Hapana na sina kinga hiyo

    Katuga: Ndugu shahidi kama nilikupata vyema ulieleza sifa nyingi kukuhusu wala sizikatai iambie mahakama hizi tuzo ulizopewa ziko kwenye form gani kama maandishi au katika hali gani.

    Lissu: Ziko katika hali ya maandishi, na ile alama yenyewe

    Katuga: Ka object flani hivi.

    Lissu: Ndio

    Katuga: Embu iambie haya matuzo yote haya umeyaleta mahakamani

    Lissu: Hapana na sina sababu ya kuyaleta.

    Katuga: Twende pole pole tutakuwa na siku saba hapa.

    Lissu: Hakuna neno

    Katuga: Wewe umeleta nini hapa

    Lissu: Maneno

    Katuga: Sasa wewe uliposema mashahidi wa jamuhuri wameleta meneno ulimaanisha nini?

    Lissu: Siwajibiki kufanya hivyo mimi nimeleta maneno sababu sina kesi ya kuthibitisha

    Katuga: Sheria inasemaje?

    Lissu: Sheria inataka mtu alete ushahidi pamoja na vithibitisho

    Katuga: Unajua usilete ujuaji

    Lissu: Yes mimi mjuaji

    Katuga: Principles gani zinakutaka ulete maneno bila vithibitisho?

    Lissu: Mimi sina wajibu wa kuthibitisha lolote.

    Katuga: Unajua kifungu cha sheria kinasema yule anasema ana wajihi fulani anapaswa kuthibitisha.

    Lissu: Ndio ninathibitisha

    Katuga: Ulisema mahakama ni chombo huru wale uliosema wameelekeza uachiwe na unakubali mahakama ni chombo huru ndani ya nchi huru ya Tanzania?

    Lissu: Ndio, Kamati ya haki za binadamu ya Umpja wa Mataifa

    Katuga: Shahidi kuna mahali popote kwenye ushahdi wako kuna umekanusha maneno haya ya tunakwenda kukinukisha kweli kweli?

    Lissu: Nimesema hivi maneno hayo ukitaka kuyaelewa unabidi usikilize hotuba yote.

    Katuga: Mimi siwezi kukuuliza una akili timamu wewe ni kaka yangu

    Lissu: Niulize tu

    Katuga: Siwezi swali langu kuna mahali umekanusha maneno haya

    Lissu: Hapana

    Katuga: Kwa maana hiyo maneno haya huyakatai

    Lissu: Siyakatai wala hayana shida.

    Katuga: Nilitaka tu hicho

    Lissu: Nimesema mara kadhaa.

  14. Lissu: Mashahidi 17 wote maelezo yao hayalingani na yaliyoletwa mahakamani

    Waheshimiwa majaji mashahdi wote waliandika maelezo na maelezo ya mashahidi 16 ni vielelezo vya ushahidi wa utetezi wangu.

    Wote 17 wametoa ushahidi kwenye kizimba hiki ushahidi wa meneno na wote wametoa ushahidi hapa mbele ya mahakama ambao haulingani na maelezo yao yaliyoletwa mahakamani.

    Wote wameongeza mambo ambayo hayapo kwenye ushahidi wao wa maandishi.

    Wameongeza yaliyokuwa kwenye maelezo yao .Waheshimiwa majaji ni ushahdi wangu kwamba ushahidi wa meneno usiolingana na ushahidi wa maneno kwenye jambo hilohilo ni ushahidi usioaminika.

    Ni ushahidi wangu kwamba ushahidi wote wa mashahidi wa upande wa mashtaka hauaminiki.

    La mwisho waheshimiwa majaji kuhusiana na huo ushahdi usio aminika, ushahidi wa P1, P2, P3, P6, P9, P12, P19 mashahidi hawa wote ni mapolisi waliandika maelezo.

    Polisi waliandika wenyewe wakajikana wenyewe, wakajishuhudia wenyewe niliwauliza hapa sheria gani inayoruhusu haya wakasema polisi ndivyo tunavyofanya.

    Sasa waheshimiwa majaji uthibitisho wa hayo ni vilelezo D1, D5, D8, D11, D15 wamejiandikia wenyewe wamejikanya wenyewe wamejishudia wenyewe wamejikanya wenyewe sababu ni mapolisi.

    Ni shahidi mmoja tu ambaye aliandika maelezo yake mbele ya polisi mwingine kama sheria inavyotaka P15 maelezo yake DD14.

    Inspeka wa Polisi Amani Michael yeye ndio alizingatia utaratibu tu.

    Wale maaskari wa kule Ruvuma nao maelezo yao yaliandikwa kwa usahihi mbele ya askari wengine, lakini hawakuletwa kuja kutoa ushahidi.

    Waheshimiwa majaji nimemaliza mtanisamehe nimevuta muda kidogo ushahidi wangu ndio huo.

    Ukawa wakati wa mapumziko....

  15. Lissu: Nilimuuliza OCCID kwanini mmenikamata na kunidhalilisha namna hii?

    Waheshimiwa majaji kuhusu ukamataji, nilikamatwa mbinga kwenye mkutano wa haadhara, Mimi ndio nilikua nahutubia mkutano nilikuwa jukwaani na kabla sijashuka jukwaani mkutano wetu unaisha saa 12 nilifuatwa na afisa wa Polisi aliyejitambulisha ndiye OCD mbinga nimemsahahu jina.

    Waheshimiwa majaji, akaniambia nakutaka kituoni sasa hivi.

    Nikamuuliza unanitakia nini wewe Polisi, nimefanya kosa gani akaniambia twende wewe utajua hayo mbele ya safari nikamwambia afande huo sio utaratibu wa kisheria wa nchi hii, niambie kosa langu tutaenda usiponiambia hatuendi, niambie kosa langu usiponiambia siendi.

    Waheshimiwa majaji huyo bwana OCD alishuka jukwaani nikaendelea kuwaaga wananchi ghafla nikasikia kishindo cha mabomu ya machozi, walipiga mabomu ya machozi mengi sana na waliwapiga watu kwa marungu sana.

    Mimi nilikua jukwaani ila sijui nilishukaje nilijikuta nimeshakalishwa chini kwemye gari ya polisi chini sakafuni sikuwa peke yangu nikapelekwa mpaka kituo cha Polisi Mbinga, walinipeleka mpaka Chumba ofisi ya OCCID sio lockup sitatoa ushuhuda wa uongo walinipeleka kwenye ofisi ya OCCID, waliponiingiza niliingizwa na mtu aliyejitambulisha kuwa yeye ndiye OCCID Lugano Gwasa super intendent wa Polisi.

    Nikamuuliza nimekaa pale karibu saa nzima waheshimiwa majaji na nilimuuliza kwanini mmenikamata na kunidhalilisha namna hii na aliniambia sisi tumeletewa amri ya kukukamata na RPC wetu, hatujaambiwa kosa lako, hilo utaenda kulijua mbele ya safari.

    Waheshimiwa majaji baada ya kukaa pale Mbinga giza likiwa limeshaingia kama saa moja nikapakiwa kwenye gari nikapelekwa mpaka Songea mjini ofisini kwa RPC na nilimkuta na nikamuuliza hawa watu wako wa mbinga wamesema wewe ndio umesema nikamatwe niambie nimetenda kosa gani?

    RPC Chilya aliniambia yeye anatekeleza amri iliyotoka makao makuu ya Polisi Dodoma ambayo ilielekeza nikamatwe nipelekwe Dar es salaam ambako kuna kesi imefunguliwa dhidi yangu na hakunieleza ni kesi gani waheshimiwa majaji.

    Waheshimiwa majaji ni RPC Chilya ndiye aliyeniambia tunakusafirisha kwenda Dar es salaam usiku huuhuu.

    Na siku hiyo muda nakamatwa hiyo jioni mimi, wenzangu tulikua tumezunguka siku nzima kufanya mikutano na tulikuwa tumechoka na hatujala kabisa nikamuomba afande ampigie dada yangu aniliteee chakula na kumpigia kaka yangu amueleze nimekamatwa na RPC Chilya hakunieleza kosa langu nitakuja kuelezwa Dar es salaam kesho yake.

    Katika orodha ya mashahidi ni pamoja Lugano Gwasa OCCID na RCO Ruvuma hawakuletwa kuja kutoa ushahidi na kama wangeletwa wangethibitisha jinsi zoezi la ukamataji lilivyokiukwa.

    Waheshimiwa majaji sehemu yangu ya mwisho ya ushahdi haitakuwa ndefu ninaelekea kumaliza.

  16. Lissu: Hiyo serikali mnayodai nimeitishia ni ipi?

    Lissu: Shahidi PW16 Amini Mahamba ambaye alichukua uongozi wa timu ya upelelezi tarehe 8, siku nne baadaye alisema alipokutana na timu na kuangalia ile video pamoja nao siku hiyohiyo alibaini kuna uhaini hakukuwa na presumption of innocence ndio maana hawakwenda usalama wa taifa kwa wanasheria yani walikuwa na majibu yao tayari.

    Na kwa vile walikuwa na majibu waheshimiwa majaji waliulizwa mmewatafuta viongozi wa Chadema muwaulize walisema hapana,

    Mlinitafuta Mimi mniulize niwaeleze ilimaanisha nini walisema hapana na haikuwa na maana sababu tayari kwao nilikuwa na kosa na kwa sababu hiyohiyo ya Polisi kuwa na majibu hata walipoletewa ushahidi na PW17 kutoka dodoma maelezo ya P yanasema yeye ndiye alichapisha na kusambaza kwao.

    Maelezo ya shahidi P hayakuwa na maana sababu tayari wao walikuwa na majibu.

    Nilimuuliza P16 kama alisoma maelezo ya baadhi ya mashahidi yanayoonesha nani alipiga zile video maelezo yanayosema ni P17 na watu wake wa Jambo ndio walirekodi kuchapisha na kusammbaza lakini kwa sababu kwao tayari nilikuwa na makosa haikuwa na maana kufuata taratibu.

    Waheshimiwa majaji ukiukaji mwingine wakati wa upelelezi niliwauliza kwenye PGO aya ya 25 ni matendo yanayoendana na makosa mpaka sheria iseme hivyo?

    Nikawauliza waangalie sheria kuwa nilikuwa na nia ya kuzuia na kuvuruga uchaguzi wakasema haipo.

    Nikawaonesha ibara ya 151 /1 ya katiba juu ya maana ya serikali, wakaona serikali ni kitu gani, nikawauliza waambieni majaji kama kwenye maneno yangu kuna serikali ya jamuhuri?... hakuna, serikali ya mapinduzi ya zanzibar?... hakuna. kuna rais wa jamuhuri hakuna kuna serikali ya halmashauri hakuna.

    Nikawauliza kuna neno mkuu wa mkoa fulani?..hakuna.

    Nikawauliza kwenye hayo maneno kuna mahali mamlaka za mji au serikali za mitaa imetajwa?.. wakasema hakuna.

    Nikawauliza kuna jina au neno linalomhusisha Rais, Makamu wake au Waziri Mkuu? wakasema hakuna.

    Nikawauliza kuna neno au jina linalomhusisha kiongozi yeyote wa serikali iwe kuu au serikali za mitaa? Nikawauliza hiyo serikali mnayodai nimeitishia ni Ipi? ..waheshimiwa majaji hawakuwa na lolote la kusema.

  17. Lissu: Niliwauliza mashahidi mnayolalamikia yanakosa gani lakini hawakuwa na cha kusema

    Lissu: Shahidi P17 anasema alikuwepo mtu mmoja alikuwa na jina la kibantu na simkumbuki na huyo mtu hakuja kutoa ushahidi kwa hiyo upelelezi wa kesi ya uhaini haukumshirikisha mwendesha mashitaka na wanasheria wake.

    Lissu: Waheshimiwa majaji shahidi namba moja namba mbili na namba 16, Amin Mahamba waliulizwa kwamba kwenye PGO mnatambua kwamba mmeelekezwa kuna haki ya kikatiba ya watuhumiwa na haki yenyewe ni kutoa maoni kujieleza, haki ya kumlinda wakasomewa wakasema ndio wanafahamu na nikawauliza mnafahamu kwenye PGO mmeamriwa kutokutoka nje ya hiyo amri wakasema wanafahamu.

    Nikawauliza waleze jinsi walivyozingatia haki zangu kama wanavyoelekezwa na PGO kuwa walizingatia haki zangu waheshimiwa majaji hawakuwa na lakusema.

    Waheshimiwa majaji mashahidi haohao PW1 PW2 na PW16 niliwaonesha mimi matakwa ya vifungu vya 52, 2:B vinavyosema ukipinga serikali, ukitoa kauli za kuishambulia serikali, ukitoa maneno ambayo katika mazingira mengine yanaweza kuwa kosa la jinai lakini ukiyatoa kwa lengo kutaka kuonesha serikali imekosea kwenye utendaji wake na kwa lengo la kutaka kubadilisha mambo vifungu hivyo viwili vinasema hujatenda kosa.

    Niliwauliza hayo maneno mnayolalamikia yanakosa gani wakati yalitolewa yakitaka kuonesha ubovu wa katiba, madhaifu kwenye mifumo na si vinginevyo na hawakuwa na chochote cha kusema waheshimiwa majaji.

    Pia niliwaonesha kifungu cha 52:2 cha sheria ya vyombo vya habari kinachosema sio kosa la jinai kusema ubovu wa katiba na madhaifu mengine ya serikali kwa nia ya kutaka kubadilisha mambo na walisema ndio waheshimiwa majaji na nikawauliza mlizingatiaje haya kwenye maelezo yenu?, mlizingatiaje vifungu hivi?', hawakuwa na ya kusema waheshimiwa majaji.

    Kadhalika niliwaonesha hawa mashahidi watatu PGO namba moja aya ya 24 ambayo inasema nguzo kuu wakati wa upelelezi wa makosa ya jinai ni presumption of innocence mfanye upelelezi mkijua mtuhumiwa hana hatia na nilipowaonesha hiyo walisema ndio ni hivyo

    Na kwenye PGO hiyo hiyo nikawaonesha Polisi wakifuata misingi mingine nje ya PGO hiyo hamtafuata taratibu sahihi za kujua ukweli na haki haitatendeka na walisema ndio ni kweli.

    Sasa waheshimiwa majaji ushahidi wa mashahidi hawa unaonesha hivi waliona ile video tarehe 4/04/2025 huo ni ushahdi wa PW1 na PW2 kosa limefanyika tarehe tatu na siku iliyofuata PW1 akampelekea PW2 na akamuonesha vipande vipande na siku hiyo hiyo akaamuru nifunguliwe jalada la uhaini yaani hakukua na wanasheria yani hakukuwa na presumption of innocence.

  18. Kuhusu ushahidi dhidi yake

    Anazungumzia ushahidi wenyewe uliotolewa na mashahidi hawa na atatoa ushahidi wake kuonesha kuwa ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka hauoneshi kuwepo kwa kosa la uhaini au kosa la jinai.

    Wakati wa PH upande wa mashtaka ulileta orodha ya mashahidi 30 ambao walisema hao ndio watakaoleta ushahidi wa kuthibitisha tuhuma za uhaini dhidi yake.

    Anasema kuwa upande wa mashtaka haukuleta Mashahidi wote hawa 30 na Badala yake walileta 17 Pekee.

    Katika Mashahidi 17 ambao walioletwa 8 ni Askari Polisi 9 waliobaki ni wa Kificho na hawa 9 mahakama haiwafahamu majina yao na wala haifahamu wanaishi wapi haifahamu wanafanya kazi gani na haifahamu chochote zaidi majina waliopewa haya ya akina P na inaweza kuwa wamekuwa hapa muda wote kesi inaendelea maana mahakama haiujui na upande wa utetezi haiwajui.

  19. Karibu katika siku nyingine ya taarifa zetu za moja kwa moja kutoka mahakamani, ambapo Tundu Lissu anatoa ushahidi wake dhidi ya upande wa mashtaka.

  20. Lissu: Kauli zangu zilinyofolewa nje ya muktadha

    Nilisema hivi: mabadiliko yanahitaji muda, na kama kweli kulikuwa na utayari wa kufanya mageuzi, basi uchaguzi ungeweza kuahirishwa ili kutoa nafasi ya kuyatekeleza. Hata hivyo, CCM ilikataa kabisa wazo hilo.

    Matokeo yake, watu waliuawa. Kwa mujibu wa Tume ya Jaji Chande, watu 518 walipoteza maisha, huku hatima ya wengine ikiwa haijulikani. Ninaamini kuwa kama uchaguzi ungeahirishwa, maafa hayo yangeweza kuepukika.

    Baadaye nikaelezwa kuwa nilisema "nitakinukisha" na kwamba nilihamasisha maandamano. Lakini maneno hayo yalinyofolewa ‘nje ya muktadha’.

    Katika mazungumzo yale, sikuzungumzia tutaifanyaje serikali hii. Hayo hayakuwa sehemu ya ajenda yangu.

    Leo ninaambiwa nilikuwa na nia ya kuitishia serikali. Ilitoka wapi? Mliambiwa na nani?

    Nia yangu ilikuwa kuwaelewesha watia nia wa chama changu kuhusu matatizo ya mfumo wetu wa uchaguzi ili waweze kuelewa na kuunga mkono msimamo wa CHADEMA wa "No Reforms, No Election".

    Haikuwa kuitishia serikali, kwa sababu hilo halikuwa lengo wala ajenda yangu.

    Sikuhamasisha watu kufanya fujo. Mimi ni mwanasheria, na hakuna sheria yenye masuala ya "kukinukisha."

    Kusudi letu lilikuwa kuwaelimisha na kuwahamasisha Watanzania nchi nzima.

    Tutakapokutana kesho kutwa, nataka niwapitishe kwenye ushahidi uliowasilishwa mbele yenu muone kama unajitosheleza kunyonga mtu.

    Kwa kuwa muda umeisha, naomba niishie hapa kwa leo. Tukutane tena Jumatano.

    Zaidi soma hapa: