Shahidi John Mnyika anatoa ushahidi wake
Pande zote mbili ziko tayari kuendelea Lissu anamwita shahidi wake wa pili.
Mnyika tayari amepanda kizimba cha shahidi anasubiri kiapo kwa mujibu wa imani yake.
Jaji: Shahidi unaitwa nani
Mnyika: John John Mnyika
Jaji: Unafanya shughuli gani
Mnyika: Katibu mkuu wa Chadema
Jaji: Dini yako
Mnyika: Mkristo
Jaji: Utaapishwa kwa mujibu wa imani yako
Myika anakula kiapo mbele ya mahakama tayari kutoa ushahidi
Lissu: Shahidi naomba nikuongeze kwenye kutoa ushahidi wako naomba ujibu pole pole na kwa sauti
Lissu: Umeshikilia nafasi hii ya katibu mkuu tangu lini?
Mnyika: Tangu mwaka 2019 Lissu waeleze majaji kabla ya nafasi hiyo ulikuwa na nafasi nyingine ndani ya chama chako.
Mnyika: Nilikua Mkurugenzi wa vijana taifa tangu mwaka 2003 Nafasi ambayo niliishikilia mpaka mwaka 2011 wakati nashikilia nafasi mwaka 2007 niliteuliwa kuwa mkurugenzi wa habari na uenezi nilikua nashika nafasi zote mbili ambazo nilizitumikia mwaka 2014
Na wakati huohuo kati ya mwaka 2009 mpaka mwaka 2011 nilishikilia pia nafasi ya ukurugenzi wa mambo ya nje na mahusiano ya kimataifa Chadema Mwaka 2014 niliteuliwa kuwa naibu katibu mkuu chadema taifa hadi 2019 nilipochaguliwa kuwa katibu mkuu Nilikua pia mbunge.
Lissu: Huko sijakupeleka bado nataka za chama kwanza
Mnyika: Nilishakuwa mwenyekiti wa chama mkoa wa kinondoni kwa vipindi viwili.
Lissu: Nafasi nyingine zaidi ya hizo..?
Myika: Nilipokuwa Mbunge wa ubungo nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa wabunge wa Chadema bungeni mwaka 2010 hadi 2015.
Na nilikuwa Mbunge wa jimbo la kibamba kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2020.
Lissu: Sasa shahidi nafasi ya katibu mkuu wa Chadema ni nafasi ya aina gani ndani ya chama.
Mnyika: Chadema inaongozwa kwa misingi ya Chadema na nafasi ya katibu mkuu ni nafasi ya Mtendaji mkuu wa Chama ambaye ndiye mwenyekiti wa sekretarieti ya chama ambacho ndio chombo kinacho simamia chama hivyo Katibu Mkuu ndiye msimamizi wa rasilimali zote za chama na shughuli zote za chama.
Lissu: Ukisikia jaji amesema mh ndio unaendelea hahahaha.
Jaji: Tuendelee.
Mnyika: Vilevile ndio msimamizi mkuu wa watumishi wote wa makao makuu ya chama na watendaji wake.
Lissu: Ahsante, sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama chama chako huwa kinafanya mikutano na taratibu za kuandaa hiyo mikutano.
Mnyika: Chama huwa kinafanya mikutano ya ndani ikiwemo vikao vya kikatiba ikiwemo mikutano ya hadhara kwa upande wa mikutano ya ndani ngazi husika ya kiutendaji ambayo ni sekretarieti inakaa kikao ngazi ya taifa chini ya katibu mkuu, kinafanya maamuzi ya kufanya kikao husika na utaratibu wa maandalizi yake.
Lissu: Kwa vikao vya ndani kama nimekuelewa kazi ya kuandaa vikao ni kazi ya sekretarieti taifa ya Chama naomba waeleze majaji nani ni wajumbe wa hiyo sekretarieti
Mnyika: Ni Katibu Mkuu, manaibu katibu wakuu wawili mmoja wa bara mwingine wa Zanzibar wakurugenzi wa kKurugenzi za Chama taifa, wataalamu, makatibu wa sekretarieti na makatibu wa mabaraza ya chama wakiongozwa na baraza la wazee, Baraza la wanawake (Bawacha) na Baraza la Vijana (Bavicha).
Lissu: Hao ndio wajumbe wa sekretarieti ya chama taifa
Mnyika: Ndio
Lissu: Katika wajumbe wote uliowataja waeleze majaji kama mwenyekiti wa chama ni sehemu ya sekretarieti ya Chama taifa.
Mnyika: Mwenyekiti sio sehemu ya sekretarieti taifa Lissu waeleze majaji kama mwenyekiti anashiriki kwenye hivyo vikao vya maandalizi.
Mwenyekiti huwa hashiriki kwenye hivyo vikao
Lissu: Leo tuko mahakamani sababu ya kesi ya uhaini inayonikabili mimi. Mimi niliitisha mkutano wa watia nia wa uchaguzi mkuu mwaka 2015, waeleze majaji kama unaufahamu huo mkutano wa Aprili tatu mwezi wa nne mwaka jana.
Mnyika: Ninaufahamu huo mkutano sababu uliandaliwa kwa maelekezo yangu na sekretarieti ambayo ninaisimamia na ilifanya maandalizi chini ya usimamizi wangu na nikishiriki mkutano wewe
Lissu: Waeleze majaji huo mkutano ulikuwa wa hadhara.
Mnyika:Ulikuwa mkutano wa ndani.
Lissu: Mkutano ulikuwa na lengo gani?
Mnyika: Ulikuwa ni mkutano wa ndani wa kutaka kufanyika kwa azimio la kimageuzi ya kikatiba na kisheria na kuwezesha kuwepo kwa uchaguzi huru na wa haki chini ya kauli mbiu ya No reforms no Election ikimaanisha bila mabadiliko hakuna uchaguzi
Lissu: Huo mkutano uliwahusu wakina nani?
Mnyika: Mkutano uliwahusu wote waliokuwa na nia ya kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 maarufu kama watia nia 2025.
Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama kuna watu wengine nje ya hao watia nia mliowashirikisha kwenye mkutano huo
Mnyika: Tulialika viongozi wakuu wa chama na waandishi wa habari
Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kusema ulialika viongozi wakuu wa chama mnaaanisha akina nani?
Mnyika: Mwenyekiti wa chama taifa.
Tundu Antipas Lissu, Makamo mwenyekiti Bara John Wegesa Heche, Makamo mwenyekiti Zanzibar Siad Mzee Said na viongozi wengine wakuu ambao ni sehemu ya manaibu wake.
Lissu: Ahsante Katibu mkuu , Shahidi huo mkutano wa ndani ulifanyikia wapi?
Mnyika: Mkutano ulifanyikia makao makuu ya chama mikocheni mtaa wa daima nyumba namba 31 kwenye ukumbi wa chama wa mikutano
Lissu: Shahidi umesema vilevile mlialika waandishi wa habari na ni wa vyombo vipi kwa kumbukumbu zako?
Mnyika: Kazi ya kualika waandishi wa habari ilifanywa na mkurugenzi wa mawasiliano wa Chama Brenda Jonas Rupia na nilielekeza itolewe taarifa kwa umma (Tangazo) ambalo lilitolewa tarehe 27 mwezi Machi ambalo lilialika waandishi wa habari na kuutarifu umma juu ya kikao hiki na ilisainiwa na Brenda Rupia.