Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Lissu anahitimisha ushahidi wake kesi ya uhaini

Upande wa Mashataka umemaliza kumuuliza maswali ya dodoso Lissu ambaye anahitimisha ushahidi wake kabla ya mashahidi wengine wa upande wa utetezi kuanza kutoa ushahidi wao

Muhtasari

Moja kwa moja

Elizabeth Kazibure, Rashid Abdallah & Asha Juma

  1. Shahidi John Mnyika anatoa ushahidi wake

    Pande zote mbili ziko tayari kuendelea Lissu anamwita shahidi wake wa pili.

    Mnyika tayari amepanda kizimba cha shahidi anasubiri kiapo kwa mujibu wa imani yake.

    Jaji: Shahidi unaitwa nani

    Mnyika: John John Mnyika

    Jaji: Unafanya shughuli gani

    Mnyika: Katibu mkuu wa Chadema

    Jaji: Dini yako

    Mnyika: Mkristo

    Jaji: Utaapishwa kwa mujibu wa imani yako

    Myika anakula kiapo mbele ya mahakama tayari kutoa ushahidi

    Lissu: Shahidi naomba nikuongeze kwenye kutoa ushahidi wako naomba ujibu pole pole na kwa sauti

    Lissu: Umeshikilia nafasi hii ya katibu mkuu tangu lini?

    Mnyika: Tangu mwaka 2019 Lissu waeleze majaji kabla ya nafasi hiyo ulikuwa na nafasi nyingine ndani ya chama chako.

    Mnyika: Nilikua Mkurugenzi wa vijana taifa tangu mwaka 2003 Nafasi ambayo niliishikilia mpaka mwaka 2011 wakati nashikilia nafasi mwaka 2007 niliteuliwa kuwa mkurugenzi wa habari na uenezi nilikua nashika nafasi zote mbili ambazo nilizitumikia mwaka 2014

    Na wakati huohuo kati ya mwaka 2009 mpaka mwaka 2011 nilishikilia pia nafasi ya ukurugenzi wa mambo ya nje na mahusiano ya kimataifa Chadema Mwaka 2014 niliteuliwa kuwa naibu katibu mkuu chadema taifa hadi 2019 nilipochaguliwa kuwa katibu mkuu Nilikua pia mbunge.

    Lissu: Huko sijakupeleka bado nataka za chama kwanza

    Mnyika: Nilishakuwa mwenyekiti wa chama mkoa wa kinondoni kwa vipindi viwili.

    Lissu: Nafasi nyingine zaidi ya hizo..?

    Myika: Nilipokuwa Mbunge wa ubungo nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa wabunge wa Chadema bungeni mwaka 2010 hadi 2015.

    Na nilikuwa Mbunge wa jimbo la kibamba kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2020.

    Lissu: Sasa shahidi nafasi ya katibu mkuu wa Chadema ni nafasi ya aina gani ndani ya chama.

    Mnyika: Chadema inaongozwa kwa misingi ya Chadema na nafasi ya katibu mkuu ni nafasi ya Mtendaji mkuu wa Chama ambaye ndiye mwenyekiti wa sekretarieti ya chama ambacho ndio chombo kinacho simamia chama hivyo Katibu Mkuu ndiye msimamizi wa rasilimali zote za chama na shughuli zote za chama.

    Lissu: Ukisikia jaji amesema mh ndio unaendelea hahahaha.

    Jaji: Tuendelee.

    Mnyika: Vilevile ndio msimamizi mkuu wa watumishi wote wa makao makuu ya chama na watendaji wake.

    Lissu: Ahsante, sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama chama chako huwa kinafanya mikutano na taratibu za kuandaa hiyo mikutano.

    Mnyika: Chama huwa kinafanya mikutano ya ndani ikiwemo vikao vya kikatiba ikiwemo mikutano ya hadhara kwa upande wa mikutano ya ndani ngazi husika ya kiutendaji ambayo ni sekretarieti inakaa kikao ngazi ya taifa chini ya katibu mkuu, kinafanya maamuzi ya kufanya kikao husika na utaratibu wa maandalizi yake.

    Lissu: Kwa vikao vya ndani kama nimekuelewa kazi ya kuandaa vikao ni kazi ya sekretarieti taifa ya Chama naomba waeleze majaji nani ni wajumbe wa hiyo sekretarieti

    Mnyika: Ni Katibu Mkuu, manaibu katibu wakuu wawili mmoja wa bara mwingine wa Zanzibar wakurugenzi wa kKurugenzi za Chama taifa, wataalamu, makatibu wa sekretarieti na makatibu wa mabaraza ya chama wakiongozwa na baraza la wazee, Baraza la wanawake (Bawacha) na Baraza la Vijana (Bavicha).

    Lissu: Hao ndio wajumbe wa sekretarieti ya chama taifa

    Mnyika: Ndio

    Lissu: Katika wajumbe wote uliowataja waeleze majaji kama mwenyekiti wa chama ni sehemu ya sekretarieti ya Chama taifa.

    Mnyika: Mwenyekiti sio sehemu ya sekretarieti taifa Lissu waeleze majaji kama mwenyekiti anashiriki kwenye hivyo vikao vya maandalizi.

    Mwenyekiti huwa hashiriki kwenye hivyo vikao

    Lissu: Leo tuko mahakamani sababu ya kesi ya uhaini inayonikabili mimi. Mimi niliitisha mkutano wa watia nia wa uchaguzi mkuu mwaka 2015, waeleze majaji kama unaufahamu huo mkutano wa Aprili tatu mwezi wa nne mwaka jana.

    Mnyika: Ninaufahamu huo mkutano sababu uliandaliwa kwa maelekezo yangu na sekretarieti ambayo ninaisimamia na ilifanya maandalizi chini ya usimamizi wangu na nikishiriki mkutano wewe

    Lissu: Waeleze majaji huo mkutano ulikuwa wa hadhara.

    Mnyika:Ulikuwa mkutano wa ndani.

    Lissu: Mkutano ulikuwa na lengo gani?

    Mnyika: Ulikuwa ni mkutano wa ndani wa kutaka kufanyika kwa azimio la kimageuzi ya kikatiba na kisheria na kuwezesha kuwepo kwa uchaguzi huru na wa haki chini ya kauli mbiu ya No reforms no Election ikimaanisha bila mabadiliko hakuna uchaguzi

    Lissu: Huo mkutano uliwahusu wakina nani?

    Mnyika: Mkutano uliwahusu wote waliokuwa na nia ya kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 maarufu kama watia nia 2025.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama kuna watu wengine nje ya hao watia nia mliowashirikisha kwenye mkutano huo

    Mnyika: Tulialika viongozi wakuu wa chama na waandishi wa habari

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kusema ulialika viongozi wakuu wa chama mnaaanisha akina nani?

    Mnyika: Mwenyekiti wa chama taifa.

    Tundu Antipas Lissu, Makamo mwenyekiti Bara John Wegesa Heche, Makamo mwenyekiti Zanzibar Siad Mzee Said na viongozi wengine wakuu ambao ni sehemu ya manaibu wake.

    Lissu: Ahsante Katibu mkuu , Shahidi huo mkutano wa ndani ulifanyikia wapi?

    Mnyika: Mkutano ulifanyikia makao makuu ya chama mikocheni mtaa wa daima nyumba namba 31 kwenye ukumbi wa chama wa mikutano

    Lissu: Shahidi umesema vilevile mlialika waandishi wa habari na ni wa vyombo vipi kwa kumbukumbu zako?

    Mnyika: Kazi ya kualika waandishi wa habari ilifanywa na mkurugenzi wa mawasiliano wa Chama Brenda Jonas Rupia na nilielekeza itolewe taarifa kwa umma (Tangazo) ambalo lilitolewa tarehe 27 mwezi Machi ambalo lilialika waandishi wa habari na kuutarifu umma juu ya kikao hiki na ilisainiwa na Brenda Rupia.

  2. Lissu akamilisha ufafanuzi wa ushahidi wake

    Kielelezo cha D14. Detective Amani Michael ndiye afisa wa polisi kati ya hawa wote pekee aliyejaza maelezo kwa usahihi. Kila sehemu kuna saini yake katika kila ukurasa, na mwisho kuna saini ya afisa wa polisi aliyemchukua maelezo na kuyaandika. Huyu tu.

    Lissu: Niliulizwa na wakili wa Serikali, Nzengeli, "Hawa mashahidi wa Jamhuri unawaita wahalifu kwani walishahukumiwa?"

    Waheshimiwa majaji, watu ambao wamepanga kufanya uhalifu wakakamatwa kwa kupanga kufanya uhalifu, wakakiri mbele ya polisi kuwa wanapanga kufanya uhalifu, wakaja mahakamani wakaiambia mahakama, walio panga kufanya uhalifu. Ni ushahidi wangu kwamba hawa ni wahalifu.

    Nzengeli: Kweli ni ushahidi wake, lakini mimi nilimuuliza kati ya wewe na mahakama nani anaweza kusema wale ni wahalifu?

    Lissu: Waheshimiwa majaji, nimetoa ufafanuzi.

    Jaji: Tuendelee.

    Lissu: Naelekea kumaliza, waheshimiwa majaji.

    Kulikuwa na maswali niliyoulizwa juu ya omission na contradiction, na kwenye jibu langu moja wapo ni kwamba hizi omission ndio contradiction zenyewe. Sijui kama kwenye rekodi ipo sahihi.

    Jaji: Kwa swali lipi?

    Lissu: Basi niondoke hapo, waheshimiwa majaji. Kwa karatasi ambazo ninazo, waheshimiwa majaji, nimemaliza.

    Jaji: Na ndio msingi wa re-examination. Huwezi kuuliza na kufafanua kila kitu.

    "Lissu amemaliza kutoa ushahidi"

    Wakati Lissu ameomba mapumziko kidogo kesi iendelee saa nane. Akiwa anarudi kizimba cha mshitakiwa alisema "Uhuruni kunaendaje? Waambie nimewamiss."

  3. Mahakama yamzuia Lissu kutoa ufafanuzi zaidi kwenye Re-examination

    Lissu: Naomba washauri wangu wanisomee swali la mwisho, sikuliandika.

    Nzengeli: Naona utaratibu unakiukwa. Hao anaowaita washauri hawatambuliki na mahakama. Kama hakuandika, aiombe mahakama.

    Jaji: Naomba tuendelee.

    Lissu: Nimeulizwa kwamba nia ya kutenda kosa inathibitishwa na matendo? Nikajibu si kweli. Ufafanuzi wangu ni huu kwenye kesi za uhaini.

    Nzengeli: Swali niliuliza mwenyewe na sikuacha nafasi ya maelezo. Swali lilifungwa, kama atatoa maelezo itabidi turudi kwenye cross-examination.

    Lissu: Hili pingamizi ni la bure. Sasa anayeamua nifafanue ni wakili wa serikali au ni mimi?

    Jaji: Wote tunajua re-examination inajikita kwenye swali lililoulizwa na si zaidi.

    Lissu: Sawa, waheshimiwa majaji. Ufafanuzi wangu ni kwamba si kweli makosa yote nia inathibitishwa kwa matendo. Makosa mengine nia inathibitishwa kwa uchapishaji.

    Jaji: Ndiyo.

    Lissu: Waheshimiwa majaji, niliulizwa na wakili...

    Katuga: Kwamba hii kesi imeshachunguzwa vilevile na Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. Ikauliza mahakama yetu iko huru? Nikajibu iko huru. Pamoja na kwamba mahakama yetu iko huru, hizo taasisi nyingine zina umuhimu wake.

    Katuga: Yaleyale, waheshimiwa majaji, sababu alijibu na wala sikuuliza habari ya umuhimu. Sasa kwa namna hii tutamaliza kesi? Ndiyo maana tukasema hii itakuwa na changamoto zake. Ufafanuzi huu anaoufanya ni kuleta ushahidi mpya na sisi tuko macho, unless aiombe mahakama alete ushahidi mpya.

    Lissu: Waheshimiwa majaji, huu si ushahidi mpya. Ameniuliza mwenyewe kama mahakama yetu inapangiwa na kama iko huru. Nafafanua wala si ushahidi mpya, waheshimiwa majaji.

    Jaji: Hili suala litatuchukua muda mrefu sana kama hatutafuata taratibu, na hata kwenye re-examination si kila swali. Hebu lisome tena hilo swali vyema.

    Lissu: Ninachotaka kusema ni kwamba mahakama zetu, licha ya kwamba hazipangiwi, hazinyimwi kutazama maamuzi ya taasisi nyingine za kimataifa.

    Katuga: Waheshimiwa majaji, yeye alishajibu iko huru. Hayo ya instruments nyingine mimi sikuuliza. Sasa kuyaleta sasa hivi halikuwa sehemu ya swali langu, mimi sikuuliza kabisa.

    Lissu: Mzigo wa kuthibitisha mashtaka ni wa upande wa waleta mashtaka.

    Jaji: Tuendelee.

    Lissu: Waheshimiwa majaji, niliulizwa vilevile kwamba kwenye ushahidi wangu nilisema kwamba niliwahi kuwa Rais wa Tanganyika Law Society. Nikasema ni kweli, na nikaulizwa uliposhtakiwa ulikuwa bado Rais wa TLS, na nikaulizwa ulikuwa na kinga. Naomba nifafanue.

    Jaji: Unafafanua nini hapo? Naomba tuendelee.

    Lissu: Niliulizwa njia ya kupinga sheria zinazokinzana na Katiba. Nimesema kuna njia za kimahakama na zisizo za kimahakama, na nikaulizwa hiyo iko kwenye kifungu gani cha Katiba. Nikasema iko kwenye kifungu cha 20, kifungu kidogo cha kwanza.

    Sasa, waheshimiwa majaji, naomba kueleza haya majibu yangu. Hizo njia za kutaka mabadiliko ya sheria, ufafanuzi wangu ni kwamba hizo njia za nje ya mahakama zinatambulika kikatiba na zimethibitishwa hivyo na mahakama.

    Lissu: Waheshimiwa majaji, nikaulizwa kama namfahamu Ishengoma Ndyanabo. Nikaulizwa alifanya nini, nikasema ninamfahamu na alikwenda mahakamani kupinga uchaguzi. Nikaulizwa kama ninamfahamu Mchungaji Mtikila ambaye aliomba mahakama itambue mgombea binafsi, na alishinda kesi Mahakama ya Afrika na mpaka sasa haijatekelezwa.

    Jaji: Sasa hapo unafafanua nini?

    Lissu: Ni sawa, waheshimiwa majaji.

    Jaji: Tuendelee.

    Lissu: Niliulizwa sana kuhusu kifungu cha 39(2)(d) kuhusu maneno yale "or" na mimi nikasema maneno haya yanafana. Wakili wa serikali alikuwa anasema maneno haya hayafanani. Ninaomba nifafanue hili, waheshimiwa majaji. "An act" or "did" ni same thing, maana yake ni matendo, na nilivyosema yanafanana nilikuwa na maana hiyo.

    Katuga: Sikwenda kwenye tafsiri na hakuna sehemu nilimuuliza tafsiri. Na hii tafsiri ameipata wapi? Wakati kwenye cross-examination hakukuwa na hilo swali, na tukasomeshana kisheria.

    Lissu: Waheshimiwa majaji, naomba mahakama itusomee rekodi ya hiki wakili wa serikali anachokisema.

    Jaji: Anasoma kile mahakama ilichokiandika, anasoma kwa Kiingereza.

    Lissu: Naendelea, waheshimiwa majaji. Niliulizwa kama ninafahamu mihimili mitatu na nikamwambia niitaje, na nikaulizwa kazi zake nikazitaja. Niliulizwa juu ya kazi za Bunge, nikasema kutunga sheria. Nikaulizwa kwa habari ya serikali, nikasema kusimamia sheria.

    Niliposema kazi ya Bunge ni kutunga sheria, sikuwa na maana kwamba hiyo ndiyo kazi pekee ya Bunge. Nikasema kazi nyingine ni kuisimamia serikali.

    Waheshimiwa majaji, kulikuwa na ushahidi wa mashahidi wa serikali ambao hawakuja kutoa ushahidi juu ya namna nilivyokamatwa, na nikasema uhalali wa kukamatwa kwangu ni suala tofauti. Kwa sababu, waheshimiwa majaji, sheria zimeweka utaratibu wa namna ya kukamata. Kama sheria ilifuatwa au la ni suala linalobishaniwa na lilihitaji kujibiwa na upande wa mashtaka.

    Soma Zaidi Hapa:

  4. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba kuhojiwa tena

    Wakili wa Serikali (Katuga): Tunaombi waheshimiwa Majaji, upande wa Jamhuri tunafahamu kuhojiwa tena ni njia moja wapo ya shahidi kutoa ushahidi na ipo kisheria na ila tunaomba kwa mujibu wa sheria shahidi ajikite kwenye yale maswali ya kuhojiwa tena na tunajua mshitakiwa ni wakili na anajiwakilisha mwenyewe ni jinsi gani atajihoji ili kufikia lengo la kutoa ufafanuzi wa majibu yake wakati wa kuhojiwa na upande wa pili, suala ambalo tunaomba Mahakama hii tuulize, shahidi ni mtu ambaye anajiwakilisha mwenyewe sasa kuhojiwa tena itafanyikaje?

    Wakili Katuga: Ajiulize maswali mwenyewe na ajijibu mwenyewe kuna hatari ya kuleta ushahidi mpya kabisa maana lengo la kuhojiwa tena ni kufafanua sasa kujiuliza mwenyewe atakuwa hakimu wa mwenendo wako mwenyewe, sasa zile kanuni zetu zinakinzana na hiki, kama angekuwa na wakili sawa ila wewe mwenyewe ujiulize na ufafanue ili kuepuka mkanganyiko Mahakama inaweza ikamuuliza kwa vile vipande ambavyo inaona vinahitaji ufafanuzi

    Jaji: Maombi yako ni nini?

    Katuga: Tunaomba Mahakama imuelekeze shahidi atoe maelezo kama itahitajika kufanya hivyo kwenye majibu yake yenye maana zaidi ya moja na sio kufungua sababu ya kutoa uwanda wa kutoka nje ya yale ambayo yanayohitaji ufafanuzi. Ni hayo tu waheshimiwa majaji

    Lissu: Waheshimiwa majaji kabla sijajibu naomba wakili mkuu wa serikali mkuu aimbie mahakama kama ameleta pingamizi ili muitolee uamuzi na kama ni ushauri tu naomba yawekeni pembeni ili nifanye kazi ya kuhojiwa tena, kwa hiyo naomba majibu hili ni pingamizi au ni nini?

    Katuga: Waheshimiwa majaji tumeiomba Mahakama irejeee kifungu na itoe mwongozo hakuna sehemu tumesema tunapinga, tumeomba mwongozo.

    Lissu: Kwa kuwa ni mwongozo naomba nijibu hayo maombi ya mwongozo, kuhojiwa tena ni haki ya shahidi aliyekuwa aliyehojiwa na upande wa pili, ndio maana kifungu alichokitaja cha 156 moja shahidi atakuwa wakwanza kutoa ushahidi na kama upande wa pili utamhoji na shahidi huyo akitaka kuhojiwa tena ni haki yake na kama ni haki alipaswa kunyamaza kimya.

    Lissu: Wakili wa serikali mkuu anasema atajiongozaje sababu hana wakili, the fact kwamba shahidi ndiye mshitakiwa na anajiwakilisha mwenyewe (ukweli kwamba shahidi ndiye mshitakiwa na anajiwakilisha mwenyewe) kitakachofanyika ni kurejea maswali yaliyoulizwa na majibu yake na kufafanua kwa hiyo hakuna chochote cha kutolea mwongozo sheria iko wapi, hii inaweza kuwa ni fursa ya kuingiza mambo mapya?

    Lissu; Utaratibu uko wazi kama kutakuwa na mambo mapya watafanya pingamizi kwa hiyo hawapaswi kuwa na hofu ya bure sasa waheshimiwa majaji hamna mwongozo wa kutoa.

    Lissu: Baada ya kusema hayo naomba niendelee.

    Jaji: Sasa hayo uliyosema si ndo muongozo wenyewe

    Lissu: Waheshimiwa majaji kama mtatoa mwongozo kwenye jambo dogo hivi tutafika tumechoka sana ila kama anahitaji kuambiwa awe macho waheshimiwa majaji.

  5. Upande wa Mashtaka wamaliza kumdodosa Lissu

    Jaji Ndunguru: Shahidi unakumbushwa kiapo chako kinaendelea

    Lissu: Sawa sawa

    Wakili Nzengeli (Upande wa serikali): Shahidi unakumbuka jana tulipoishia naomba nikuulize swali moja la mwisho tuachane na wewe

    Lissu: Asante mmening'ang'ania sana

    Wakili wa Serikali- Nzengeli: Ni kweli au si kweli nia ya kutenda kosa inathibitishwa na matendo husika

    Lissu: Sio kweli

    Wakili Nzengeli: Waheshimiwa tulikuwa na hilo tu kwa shahidi huyu tunaomba kusema tumemaliza kwa shahidi huyu

    Upande wa Jamhuri umemaliza kumuuliza maswali Shahidi wa Kwanza wa utetezi, ambaye pia ni mshitakiwa katika kesi hiyo.

    Baada ya kukamilika kwa dodoso hilo, Tundu Lissu anatarajiwa kupewa nafasi ya kufanya majumuisho ya utetezi wake.

    Baada ya majumuisho hayo, mahakama itaendelea na hatua inayofuata ya kusikiliza ushahidi wa shahidi mwingine.

  6. Katika Picha: Matukio ya kabla ya kuanza kwa kesi ya Tundu Lisuu

  7. Kilichojiri jana Mahakamani

    Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, iliendelea jana katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam, huku upande wa serikali ukiendelea kumuhoji Lissu kuhusu ushahidi alioutoa katika utetezi wake.

    Mawakili wa serikali walimhoji Lissu kuhusu kampeni yake ya “No Reforms, No Election”, wakitaka kujua kama mkutano alioufanya ulihitaji taarifa kwa polisi na kama ulikuwa unahusiana na uchaguzi.

    Lissu alisisitiza kuwa huo ulikuwa mkutano wa ndani na kwamba mikutano ya aina hiyo haihitaji kibali.

    Sehemu nyingine ya maswali ilijikita katika kauli za Lissu kuhusu mahakama.

    Wakili wa serikali Job Mtemba alimuuliza kama kauli kwamba majaji ni CCM na kwamba “mahakamani hapaendeki” ilikuwa na lengo la kupandikiza chuki dhidi ya mfumo wa utoaji haki.

    Lissu alikataa kauli hiyo na akasema alikuwa akizungumzia masuala ya uchaguzi.

    Lissu pia alikiri mbele ya mahakama kwamba uanaharakati na uanasiasa vina mipaka ya kisheria, na kwamba hakuna kinga inayomruhusu mwanaharakati au mwanasiasa kuvunja sheria.

    Hata hivyo, alisisitiza kuwa wananchi wana haki ya kupinga uchaguzi ambao wanaona si huru wala wa haki.

    Maswali mengine yalihusu video inayodaiwa kuwa na maneno yaliyosababisha kufunguliwa kwa kesi hiyo.

    Lissu aliendelea kusisitiza kuwa video hiyo ilipaswa kuwasilishwa mahakamani, akisema mashahidi waliodai kuiona na kuisikia hawawezi kuthibitisha kikamilifu yaliyomo bila kuwepo kwa video yenyewe.

    Katika sehemu nyingine, Lissu alihoji uaminifu wa baadhi ya mashahidi wa polisi na akaeleza kuwa hakuridhishwa na namna alivyokamatwa.

    Alisema baadhi ya malalamiko yake kuhusu kukamatwa na madai ya kushambuliwa hayakushughulikiwa na polisi, huku upande wa serikali ukimhoji kwa nini hakuchukua hatua nyingine za kisheria.

    Maswali ya upande wa serikali yaliendelea hadi mahakama ilipoahirisha mwenendo wa kesi hiyo.

    Leo kesi inatarajiwa kuendelea, Lissu akiendelea kujibu maswali ya dodoso kutoka kwa upande wa Jamhuri.

  8. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya kesi ya uhaini ya Tundu Lissu, tarehe 28/08/2026.

  9. Nzengeli ahoji uhalali wa kampeni ya ‘No Reforms, No Election’

    Nzengeli: Ni kweli kwamba wakati unafanya huo mkutano wa kuzuia uchaguzi hukuwa na kibali?

    Lissu: Mikutano ya ndani haihitaji kibali, inahitaji taarifa tu.

    Nzengeli: Hapo hukupi PGO?

    Lissu: Ndiyo.

    Nzengeli: Soma kifungu cha 40(3).

    Lissu: 40(3), aya gani?

    Nzengeli: Wakati natafuta, soma Sheria ya Vyama vya Siasa.

    Lissu: Nisaidie kusoma ili tusipoteze muda.

    Nzengeli: Soma kifungu cha 40(2), aya ya sita.

    Lissu: (Anasoma.)

    Nzengeli: Wewe umekielewaje?

    Lissu: Nilichoelewa ni kwamba wakati wa mikutano ya kampeni, wanasiasa watatoa taarifa kwa polisi.

    Nzengeli: Ni kweli au si kweli mkutano huo ulikuwa unazungumzia mambo ya uchaguzi?

    Lissu: Haukuwa mkutano wa kampeni, na uchaguzi ulikuwa bado miezi sita mbele.

    Nzengeli: Waheshimiwa majaji, ninaomba nimpe Sheria ya Vyama vya Siasa, kifungu cha 23.

    Lissu: Nisomee.

    Nzengeli: (Anasoma.)

    Lissu: Ahsante, uliza swali.

    Nzengeli: Je, kwa kifungu hiki ulipaswa kupeleka taarifa polisi?

    Lissu: Hapana, si kweli, kwa sababu ulikuwa mkutano wa wazi na ulikuwa mkutano wa ndani.

    Nzengeli: Shahidi, elewa swali.

    Lissu: Mikutano ya ndani, dada yangu, haihitaji notification.

    Lissu: Next.

    Nzengeli: Ni kweli au si kweli huo mkutano unaouita wa ndani ulikuwa na waandishi wa habari?

    Lissu: Ni kweli.

    Nzengeli: Ambao ulikuwa mubashara na kila mtu aliuona?

    Lissu: Ndiyo, ni mkutano wa ndani.

    Nzengeli: Una kifungu chochote kinachokupa ruhusa ya kufanya mkutano wa ndani?

    Lissu: Kifungu hicho hicho, kwa sababu hakuna mkutano unaohitaji ruhusa bali taarifa tu. Next.

    Nzengeli: Wewe usinipangie.

    Nzengeli: Je, maneno yaliyoko kwenye hati yako ya mashtaka unakiri uliyaongea?

    Lissu: Nimesema sijatangaza maneno ya uhaini mbele ya waandishi wa habari.

    Nzengeli: Uliyaongea au hukuyazungumza? Naomba uwaangalie majaji.

    Lissu: Nimeshitakiwa kwa kuchapisha maneno yanayodaiwa kuwa ya uhaini kwa zaidi ya saa tatu.

    Nzengeli: Uliyaongea au hukuyazungumza?

    Lissu: Nimeongea kwa zaidi ya saa tatu.

    Nzengeli: Je, ni kweli video ni kifaa tu kinachotumika kuchapisha?

    Lissu: Hiyo inahitaji wataalamu.

    Nzengeli: Kati yako na mahakama, nani anaweza kusema nani ni mhalifu?

    Lissu: Mahakama ndiyo inaweza kusema mtu huyu ni mhalifu.

    Nzengeli: Na ni kweli kwamba hujaleta namba za kesi za hao mashahidi wote ambao unasema ni wahalifu?

    Lissu: Mapolisi si walifuta?

    Nzengeli: Tuhuma ni shtaka au si shtaka?

    Lissu: Tuhuma si shtaka.

    Nzengeli: Shahidi, nimekusikia ukilalamika kuhusu mambo ya kukamatwa. Uliyapeleka hayo malalamiko mahakamani?

    Lissu: Niliyapeleka na hakimu wa mahakama niliyemkabidhi alikataa. Ulitaka nifanyaje wakati niko gerezani?

    Nzengeli: Unakubali kwamba sheria zote zilizotungwa na Bunge zinasimamiwa na Serikali?

    Lissu: Sheria ya uchaguzi inasimamiwa na Tume ya Uchaguzi, si Serikali.

    Nzengeli: Kwa hiyo sheria ya uchaguzi ni sheria kama sheria nyingine?

    Lissu: Ni sheria.

    Nzengeli: Ni kweli kwamba kuna tofauti kati ya kupinga uchaguzi na kuzuia uchaguzi?

    Lissu: Waheshimiwa majaji, sisi tulitaka kupinga uchaguzi mpaka mabadiliko yafanyike. Shughuli zote za uchaguzi, majimbo yasitangazwe, wagombea wasitangazwe, kwa ujumla kila kitu kisimame.

    Lissu: Utaratibu wetu wa saa kumi na moja umekuwa suspended.

    Jaji: Ngoja tuulize, tulikuwa tunajua anamalizia.

    Nzengeli: Kwa maelezo ya mshtakiwa, ni kweli amechoka na kibinadamu. Tunaomba tuahirishe.

    Lissu: Kesho nayo ni siku.

    Jaji: Tunaahirisha shauri mpaka kesho saa tatu asubuhi.

  10. Job ambana Lissu: “Je, ulipandikiza chuki dhidi ya mahakama?”

    Job: Kwa mujibu wa ushahidi ulioutoa mbele ya mahakama hii, ulisema majaji ni wa CCM na kwamba mahakamani hapaendeki. Je, ni sahihi kwamba kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya mfumo wa utoaji haki ni kosa kwa mujibu wa sheria zetu?

    Lissu: Kupandikiza chuki ni kufanya nini? Kupandikiza chuki ni kitu gani?

    Job: Hebu soma kifungu cha 52(1).

    Lissu: (Anasoma.)

    Job: Je, utakubaliana na mimi kwamba kwa maneno yako uliyoyatoa, ukisema majaji ni wa CCM na kwamba huko mahakamani hapaendeki, ulikuwa unapandikiza chuki?

    Lissu: Waheshimiwa majaji, sikubaliani na wakili.

    Job: Je, ni sahihi kwamba Mahakama Kuu ilishawahi kutoa amri ya ulinzi wa mashahidi?

    Lissu: Ndiyo.

    Job: Na swali lingine, je, ni sahihi kwamba shauri lililoamuru utolewaji wa ulinzi wa mashahidi ni tofauti na shauri hili?

    Lissu: Ni sahihi.

    Job: Na ni sahihi kwamba amri hiyo haijawahi kuondolewa na mahakama?

    Lissu: Ni sahihi.

    Job: Kama hukuridhishwa na amri hiyo, si ulikuwa na nafasi ya kuipinga, lakini hukuchukua hatua yoyote?

    Lissu: Hapana, sikuchukua hatua kwa sababu niko gerezani. Nitapigana vita ngapi?

    Job: Hao mashahidi unawakumbuka?

    Lissu: Niwakumbukeje wakati siwajui? Ninazikumbuka hizi herufi tu.

    Job: Ukiwa kama mwanasheria...

    Lissu: Mimi ni shahidi. Uliza swali kwa shahidi.

    Job: Utakubaliana na mimi kwamba uamuzi wa ulinzi wa mashahidi hauwezi kupingwa kupitia shauri hili?

    Lissu: Sikubaliani na wewe.

    Job: Ulieleza mahakama hii kwamba tarehe 12 Agosti 2024 ulipata pigo. Kuna kitu chochote uliwasilisha hapa mahakamani kama kielelezo?

    Lissu: Nilieleza kwa mdomo.

    Job: Ulieleza mahakama tarehe 23 Septemba 2024 kwamba ulivamiwa nyumbani kwako na Jeshi la Polisi. Je, ni sahihi kwamba hakuna ushahidi mwingine ulioutoa mahali pengine?

    Lissu: Nimeieleza mahakama hii hayo, na hakuna sehemu nyingine nilikotoa ushahidi huo.

    Job: Ulieleza mahakama hii kwamba PW1 George Bagemi alitoa maelezo kuhusu wewe kufunguliwa jalada.

    Lissu: Ndivyo yeye mwenyewe alivyosema.

    Job: Je, ni sahihi kwamba PW1 alitoa maelezo kuhusu kufunguliwa majalada mawili ya uchunguzi yenye namba zifuatazo... Utakubaliana na mimi kwamba wewe, ukiwa shahidi, hujui tofauti ya majalada hayo mawili?

    Lissu: Sijui sababu. Haiko kabisa kwenye notisi zangu. Nitajuaje wakati sikuiandika?

    Job: Katika kutokujua huko sasa, uliieleza mahakama hapa kwamba PW1, baada ya kuonyeshwa video na PW2, alipoamuru kufunguliwa kwa jalada la uchunguzi, hakukosea?

    Lissu: Sababu alipaswa amweleze DPP acoordinate uchunguzi wa masuala haya, na hakumwambia.

    Job: Kifungu gani?

    Lissu: Sina hapa, ila utaratibu uko hivyo. DPP ndiye msimamizi wa upelelezi wa masuala haya, na hayo majalada mengine unayoniambia siyafahamu kabisa.

    Job: Wakati wa kujitetea uliambia mahakama kufunguliwa kwa jalada hilo ilikuwa kinyume cha sheria, kwani kufunguliwa kwa jalada hilo kulikufanya uwe na hatia.

    Lissu: Walikuwa na majibu tayari, ndiyo maana walikuwa wanasema kosa la kwanza.

    Job: Hebu waambie majaji, ni chombo kipi chenye mamlaka ya kuamua nani ana hatia na nani hana hatia?

    Lissu: Ni mahakama.

    Job: Kwa hiyo utakubaliana na mimi kwamba jalada hili ambalo PW1 alielekeza lifunguliwe kwa ajili ya uchunguzi, ilikuwa si makosa kwa maneno aliyoyasema?

    Lissu: Ndiyo, sababu tayari walishaniamua nina makosa.

    Job: Ni wakati gani mshtakiwa anakutwa na hatia?

    Lissu: Ni baada ya mahakama kufanya maamuzi.

    Job: Je, mahakama hii tayari imeshaamua?

    Lissu: Hapana.

    Job: Waheshimiwa majaji, ninaomba kuishia hapo.

  11. Lissu: Watu wafuate sheria, lakini si kila mgogoro hukimbiliwa mahakamani

    Job: Wakati unatoa utetezi wako, ulieleza mahakama hii kwamba huwezi kuwa Rais wa TLS kama wewe ni mtu wa hovyo hovyo. Na wakati unashitakiwa tarehe 25, ulikuwa Rais wa TLS?

    Lissu: Hapana.

    Job: Kwa hiyo, baada ya kutoka kuwa Rais wa TLS unaweza kuwa mtu wa hovyo?

    Lissu: Mimi si mtu wa hovyo, hata kidogo.

    Job: Baada ya kukutwa una kesi ya kujibu, umekaribia kuwa mtu wa hovyo?

    Lissu: Mimi si mtu wa hovyo, hata kidogo.

    Job: Umewahi kuandika maelezo polisi kuhusu kushambuliwa kwako?

    Lissu: Hapana. Wamekataa, licha ya kushambuliwa. Wamekataa tangu nilipokuwa Nairobi, na ulinzi nikaondolewa.

    Job: Wewe si ulijinasibu kuwa mwanasheria?

    Lissu: Una shaka na hilo?

    Job: Mimi nauliza maswali kwa mujibu wa sheria. Waheshimiwa majaji, naomba mshitakiwa atusomee kifungu cha 1 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

    Lissu: (Anasoma.).

    Job: Kwa mujibu wa hicho kifungu, wewe unakielewaje?

    Lissu: Kina maana kwamba taarifa ya makosa ya jinai inaweza kutolewa kwa afisa wa polisi, kwa maneno au kwa maandishi, kuhusu kosa au taarifa za kosa.

    Job: Utakubaliana na mimi kwamba jinai haifi?

    Lissu: Niliporudi, nilikwenda kwa RPC Dodoma nikamwambia nimekuja nichukueni maelezo. Walikataa. Nikawaambia wanipatie gari yangu.

    Job: Umeleta chochote kama ushahidi kuhusu wewe kushambuliwa?

    Lissu: Nimeieleza mahakama.

    Job: Umesema wewe ulikuwa mwanaharakati kwa muda. Je, utakubaliana na mimi kwamba unapopata taarifa za vitisho au uvunjifu wa sheria, unatakiwa kutoa taarifa kwa polisi?

    Lissu: Huwezi kutoa taarifa polisi kama vitisho vyenyewe vinatoka polisi. Ramadhani Kingai na hawa polisi wanaotoa ushahidi, hawa lao ni moja.

    Job: Utakubaliana na mimi kwamba, kwa mujibu wa Katiba, mahakama inaongozwa kwa kufuata misingi ya haki?

    Lissu: Ndivyo Katiba inavyosema.

    Job: Na utakubaliana na mimi kwamba wananchi wa Tanzania, na watu wanaoishi hapa, inapotokea mgogoro sehemu yao ya kukimbilia ni mahakamani?

    Lissu: Inategemeana na mgogoro. Kama ni wa kisheria, wanakimbilia mahakamani; kama ni wa kidini, wataenda makanisani au misikitini; kama ni wa kisiasa, wanamaliza kisiasa.

    Job: Utakubaliana na mimi kwamba si sahihi kusema mahakama haifanyi haki kwa mujibu wa Katiba?

    Lissu: Sikubaliani na wewe. Tume ya Warioba ilisema majaji hawatendi haki.

    Job: Hiyo taarifa ya Warioba umeileta hapa?

    Lissu: Ripoti ilieleza wazi kwamba baadhi ya majaji hawatendi haki na kwamba kuna rushwa mahakamani.

    Job: Wewe, kwa namna unavyoamini, watu wasifuate mfumo wa kimahakama?

    Lissu: Hapana. Watu wafuate sheria.

  12. Lissu: Uanaharakati na uanasiasa havitoi kinga ya kuvunja sheria

    Job: Hebu waambie majaji, hakuna mahali sheria zetu zinaruhusu watu kujichukulia sheria mkononi, kuchoma mali za watu au kuharibu uchaguzi.

    Lissu: Hakuna sheria inayoruhusu watu au mtu kujichukulia sheria mkononi, ila uchaguzi usio huru wala wa haki ni haki ya wananchi kuuzuia.

    Job: Hivi ukiwa mwanaharakati una kinga ya kutofuata sheria?

    Lissu: Hakuna kinga ya namna hiyo.

    Job: Vivyo hivyo ukiwa mwanasiasa?

    Lissu: Hakuna kinga ya mtu kutofuata sheria.

    Job: Wakati unajitetea, ulieleza mahakama hii kwamba kesi hii ni ya kisiasa. Wewe umeshitakiwa kama Tundu Lissu au kama mwanasiasa?

    Lissu: Nimeshitakiwa kama Tundu Lissu. Nisingekuwa mwanasiasa, nisingekuwa hapa. Nisingekuwa Mwenyekiti wa Chadema, nisingekuwa hapa.

    Job: Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, kuna sehemu umeshitakiwa kama mwanasiasa?

    Lissu: Hati haisemi hivyo, ila mashahidi wote wanasema mwenyekiti wa Chadema, mwenyekiti wa Chadema, mwanasiasa. Maelezo yote yanasema hivyo.

    Job: Utakubaliana na mimi kwamba katika ushahidi wako huu ulioutoa mbele ya mahakama hapa, hujaieleza mahakama ulishitakiwa kwa kesi gani na namba gani?

    Lissu: Hapana, sikubaliani na hilo. Nimesema kesi namba, ila ndiyo sijaitaja..

    Job: Ni kweli au si kweli ulitaja namba? Hukuitaja?

    Lissu: Ni kweli, namba sikuitaja. Ukitaka nikukumbushe, nitakukumbusha.

    Job: Utanikumbusha baadaye.

  13. Lissu akiri uanaharakati una mipaka ya kisheria mahakamani

    Job: Je, ni kweli au si kweli kwamba wewe ni mwanaharakati, na ulianza lini harakati zako?

    Lissu: Nimekuwa mwanaharakati siku nyingi, tangu nilipokuwa shule ya sekondari, baadaye jeshini na kwingineko.

    Job: Hebu waeleze majaji, uanaharakati ni nini?

    Lissu: Ni mtu anayefanya mambo au jambo fulani kupigania kitu fulani.

    Job: Ulijitambulisha pia kuwa wewe ni mwanasheria. Huu uanaharakati uliokuwa ukifanya unatambulika kwa mujibu wa sheria za nchi yetu?

    Lissu: Ndiyo, unatambulika.

    Job: Hebu wasaidie majaji. Ni kifungu gani na sheria gani mahsusi inayoutambua?

    Lissu: Katiba yetu imetoa uwanda mpana kwa wananchi kupigania mambo ambayo tunaona yanastahili kupiganiwa.

    Job: Tunaomba shahidi atuonyeshe na atusomee ibara hiyo.

    Lissu: Nimesema...

    Job: Nimesema tusomee kifungu hicho kinachoruhusu kufanya harakati.

    Lissu: Katiba haiko hivyo, ila inatupa uhuru wa kufanya harakati.

    Job: Harakati unazozifanya zina mipaka ya kisheria?

    Lissu: Ndiyo, zina mipaka ya kisheria.

    Job: Je, unakubali kwamba unapotafuta haki za upande mmoja, hutakiwi kubughudhi haki za upande mwingine?

    Lissu: Sahihi, hilo ninafahamu.

    Job: Sasa hebu waambie waheshimiwa. Kama nimekusikia vizuri, wakati unaongozwa ulikubali kwamba yale maneno yaliyomo kwenye hati ni sahihi?

    Lissu: Ni sahihi.

    Job: Sasa utakubaliana na mimi kwamba waliyosikia yale maneno waliyatafsiri kadiri yalivyo?

    Lissu: Sina hakika.

    Soma Zaidi:

  14. Katuga ahoji msimamo wa Lissu kuhusu ushahidi wa polisi

    Katuga: Waheshimiwa majaji, tunaendelea na ushahidi wa PW16, ushahidi wa Amini Mahamba. Sasa shahidi, hebu iambie mahakama kama ni ushahidi wako kwamba wapelelezi hawajakupa nafasi au hawajakupa maana ya maneno yaliyoandikwa kwenye hati ya mashtaka.

    Lissu: Huo ndio ushahidi wangu.

    Katuga: Kama unakumbuka, wakati shahidi PW1 alisema ulipofikishwa kwake, anasema alikupa nafasi ya kukuhoji ili umwelezee kuhusu maneno yako.

    Lissu: Wala hakuniuliza maana ya hayo maneno. Si kweli. Aliniambia anataka kuchukua maelezo yangu tu.

    Katuga: Na wewe ulijibu nini?

    Lissu: Nilimjibu kwamba kwa kuwa mmeshanikamata na mmeshanishtaki, tutakutana mahakamani.

    Katuga: Waambie hawa majaji, hawa wapelelezi walikupa nafasi ya kukuhoji au la.

    Lissu: Hawakunipa nafasi kwa sababu tayari nilikuwa nimeshashtakiwa.

    Katuga: Kwa hiyo ni uelewa wako wa kisheria kwamba mtuhumiwa hakamatwi?

    Lissu: Mimi nilikamatwa, nikawaambia tutakutana mahakamani.

    Katuga: Ulizuiwa na nini kutoa maana ya maelezo yako?

    Lissu: Walitaka maelezo yangu ya nini wakati walikuwa wameshanikamata?

    Katuga: Je, pale ulipokuwa, ulishindwa na nini kumpa tafsiri ya maneno hayo na Bwana Bagemi alikupa nafasi ya kutoa maelezo?

    Lissu: Ningesema nini wakati nilikuwa nimeshashtakiwa? Nimeshtakiwa kwa kosa la kifo na watu walionitesa kwa miaka 24. Ulitaka nijieleze tu?

    Katuga: Ulisema maelezo D1 hadi D16 ni vielelezo vya utetezi wako, na nakumbuka katika utetezi wako ulirejea Kielelezo D15. Waambie majaji, ni kielelezo ambacho ulikiamini na kukirejea katika utetezi wako?

    Lissu: Maneno yapi? Sikumbuki.

    Katuga: Baada ya kuunda timu, mimi na timu nzima tulitazama na kusikiliza video hiyo ambayo bado ilikuwa mtandaoni, na kama nilivyotafsiriwa nikabaini kosa la kwanza ni uhaini na kuchapisha mtandaoni. Ukaambia mahakama kuwa PW16 tayari alikuwa amekuhukumu kwa uhaini.

    Lissu: Niliyarejea nikiunganisha na ushahidi wa PW1 na PW17.

    Katuga: Kwa hiyo, kwa mujibu wa maneno ya shahidi huyu, aliona uhaini kwenye kielelezo chake au hakuona uhaini?

    Lissu: Sikusema ninawaamini. Mimi siwaamini polisi hawa.

    Katuga: Umechukua maelezo ya mashahidi wawili tofauti kwa sababu uliwaamini na ukawaambia majaji kwamba maelezo yao yanatofautiana?

    Lissu: Mimi niwaamini polisi? Hapana. Mimi niliyatoa kwa sababu yana tofauti; mmoja ameona uhaini, mwingine hajaona.

    Katuga: Unajua nimekuuliza swali la kwanza. Je, hiki ni kielelezo chako cha utetezi kwa sababu unakiamini?

    Lissu: Niliomba kiwe kielelezo changu kwa sababu kinatofautiana na maelezo mengine kwa kuwa kinaonyesha mgongano wa maelezo (contradiction).

    Katuga: Kwa maelezo yako mwenyewe sasa, shahidi, uko timamu?

    Lissu: Wewe unanionaje?

    Katuga: Wewe iambie mahakama.

    Lissu: Move on.

    Katuga: Maelezo haya unayaamini au huyaamini?

    Lissu: Niyaamini kwa jambo gani?

    Katuga: Waambie majaji kama uliwaomba kwamba maelezo yaliyomo kwenye vielelezo hivi vyote yaweze kutumika.

    Lissu: Nimejibu hilo swali. Move on.

    Katuga: Waambie majaji vielelezo D1 mpaka D15 vitumike kuonyesha nini?

    Lissu: Vitumike kuonyesha omissions na contradictions.

    Katuga: Kwa kuwa umeiambia mahakama vielelezo hivi vitumike, je, kuna sehemu umesema vielelezo vitumike hapa na visitumike pale?

    Lissu: Waheshimiwa majaji, hilo nitalifanya wakati wa kuwasilisha hoja zangu za mwisho.

    Katuga: Swali ni, uliwaambia au hukuwaambia majaji?

    Lissu: Nitawaambia wakati wa kuwasilisha hoja zangu za mwisho.

    Katuga: Waheshimiwa majaji, naomba swali hilo lirudiwe na lijibiwe.

    Lissu: Sikuwaambia.

    Katuga: Je, ni haki ya mahakama kutumia vielelezo vyako?

    Lissu: Sasa hilo ni uamuzi wa mahakama kuona namna itakavyotumia vielelezo hivyo.

    Katuga: Waheshimiwa majaji, ikiwapendeza, naomba niishie hapa na nimkaribishe wakili mwenzangu wa serikali.

    Soma Zaidi:

  15. Lissu ang’ang’ania video iletwe mahakamani, Katuga apinga hoja

    Katuga: Kwenye ile video unachokiona ni nini, maneno au video?

    Lissu: Sijaiona, si hamjaileta?

    Katuga: Katika sheria ya ushahidi, mtu akikutolea ushahidi wa maneno, anatoa ushahidi wa kusikia?

    Lissu: Ndiyo, wa kusikia kama ni wa maneno tu, ila kama ni video ni wa kuona na kusikia.

    Katuga: Unatuhumiwa kufanya nini?

    Lissu: Kutoa maneno na kuyachapisha.

    Katuga: Umewaambia majaji kwamba upande wa Jamhuri haujathibitisha shtaka hilo kwa sababu video hawajaileta. Waambie mashahidi wa Jamhuri walisemaje.

    Lissu: Walisema wameona video na kusikia maneno.

    Katuga: Kwa hiyo waliona na kusikia?

    Lissu: Huwezi kutenganisha video na sauti, kwa hiyo lazima iwe kuona na kusikia.

    Katuga: Unajua kwamba kila shahidi ana haki ya kuaminiwa?

    Lissu: Ndiyo, ninajua, na anastahili kuaminiwa kama kuna misingi ya kumuamini.

    Katuga: Sasa iambie mahakama hii, katika mashahidi wa Jamhuri wale waliosema wameona video, ni kifungu kipi kinaelekeza kwamba lazima walete video hiyo mahakamani licha ya kwamba wameiona?

    Lissu: Lazima wailete mahakamani ili waaminike.

    Katuga: Iambie mahakama, ni kweli kwamba mtu anayepandisha video mtandaoni anaweza kuja kuifuta?

    Lissu: Ndiyo.

    Katuga: Unaelewa kwamba kitu fulani kinaweza kupotea ghafla. Kama mtu atakuwa amefanya kosa kwa kupandisha video yenye tatizo kisha akaifuta, iambie mahakama kwamba mtu huyo hawezi kuja mahakamani kutoa ushahidi? Kwa hiyo kilicholetwa hapa ni nini?

    Lissu: Maneno na video havitengani. Video yenyewe haijaletwa.

    Katuga: Tuiombe mahakama ikuchukulie wewe ni muongo?

    Lissu: Jaji alisema hakumbuki, tuendelee.

    Katuga: Unataka shahidi PW17, ambaye alisema alikusikia ukisema hayo maneno ya kukinukisha, ayalete hapa mahakamani?

    Lissu: Ndiyo, ayalete hapa.

    Katuga: Ni ushahidi wako kwamba mashahidi kutoka polisi waliandika maelezo yao wenyewe na kwa hiyo si wa kuaminika? Sasa mashahidi hawa wasiaminiwe kwa sababu wameandika maelezo wenyewe. Ni kifungu gani kinaipa mahakama mamlaka hayo?

    Lissu: Kifungu cha 11 kinaelekeza kwamba polisi ambao hawakufuata utaratibu hawaaminiki.

    Katuga: Wasomee majaji.

    Lissu: (Anasoma.)

    Katuga: Waambie majaji, kwa mujibu wa kifungu hicho, kimeeleza nini kuhusu polisi anayefanya upelelezi; anapaswa kuandika maelezo?

    Lissu: Kama afisa huyo ni shahidi, basi haandikiwi maelezo.

    Katuga: Afisa mdogo wa polisi anaweza kumwandikia afisa wa juu maelezo?

    Lissu: Ndiyo, anaweza.

    Katuga: Unajua kwamba maelezo ya shahidi yanaandikwa kwa mujibu wa sheria?

    Lissu: Sikumbuki.

    Katuga: Unajua kwamba tamko ni tamko la kiushahidi, na unajua kwamba shahidi lazima aonywe?

    Soma Zaidi Hapa:

  16. Lissu ajibu maswali kuhusu ushahidi wa video

    Katuga: Kama uliwaambia majaji hawa waendesha mashtaka hawajaleta video na kwamba, kwa kuwa mahakama haina video hiyo, wameshindwa kuthibitisha mashtaka yao, waambie majaji kama wakati unasema hayo ulikuwa unajua au umesoma mashtaka yanayokukabili.

    Lissu: Nilikuwa nimesoma mashtaka yanayonikabili na niliyaelewa kwa undani.

    Katuga: Kwa mujibu wa mashtaka, kuna sehemu unashtakiwa kwa kuchapisha video?

    Lissu: Nashtakiwa kwa kuchapisha maneno kwenye mtandao wa Jambo TV.

    Katuga: Je, nitakuwa sahihi nikisema video unasikia na kuona kama video hiyo ina maneno?

    Lissu: Video ni kuona na kusikia. Kwa mujibu wa sheria ya ushahidi, mtu akitoa ushahidi kuhusiana na maneno anakuwa ametoa ushahidi wa kusikia.

    Katuga: Kwa mujibu wa mashtaka, unatuhumiwa kuyachapisha na kutoa maneno kwenye mtandao wa YouTube wa Jambo TV. Uliiambia mahakama kuwa upande wa Jamhuri haujathibitisha mashtaka kwa sababu video hiyo hawajaileta?

    Lissu: Mashahidi wote wa Jamhuri walisema kuwa wameona na kusikia maneno.

    Katuga: Unafahamu kwamba kila shahidi ana haki ya kuaminiwa isipokuwa kama mahakama ina sababu za kutomuamini, na sababu hizo lazima zionyeshwe? Iambie mahakama hii, wale mashahidi waliosema wameona video, ni kifungu gani cha sheria kinachosema kuwa ili waaminiwe lazima walete video?

    Lissu: Si lazima sheria iseme hivyo, bali hiyo ni common sense.

    Katuga: Ni kweli kwamba mtu anayeipandisha video mtandaoni ana uwezo wa kuifuta?

    Lissu: Ana uwezo huo.

    Katuga: Je, mtu akiwa amefanya kosa kwa kuchapisha video mtandaoni halafu akaifuta, na mtu mwingine akaiona video hiyo kabla haijafutwa, ni ushahidi wako kwamba hawezi kuthibitisha alichoona?

    Lissu: Hawezi kuthibitisha.

    Katuga: Video na maneno, kilicholetwa hapa mahakamani ni nini?

    Lissu: Wameleta maneno tu, na hayo si maneno ya kwenye video, kwa sababu maneno ya video huwezi kuyatenganisha na video yenyewe.

    Katuga: Unakumbuka PW17 ndiye shahidi pekee aliyekuwa live eneo la tukio?

    Lissu: Ndiyo.

    Katuga: Unakumbuka shahidi PW17 alisema Lissu alisema atauzuia uchaguzi?

    Lissu: Sikumbuki.

    Katuga: Kwa kuwa shahidi alikuwa eneo hilo, alihitajika kuileta video hiyo?

    Lissu: Alipaswa kuileta video hiyo.

    Katuga: Anasema alikusikia ukisema unaenda kuzuia uchaguzi na kwamba utaenda kukinukisha. Je, unataka shahidi huyo alete video hapa mahakamani?

    Lissu: Ndiyo, lazima.

    Katuga: Ni ushahidi wako kwamba mashahidi kutoka Jeshi la Polisi hawaaminiki kwa sababu waliandika maelezo bila kufuata utaratibu?

    Lissu: Ni kweli hawaaminiki kwa sababu hawakufuata utaratibu.

    Katuga: Ni kweli kwamba mashahidi wote uliowataja walikuja hapa mahakamani kutoa ushahidi, na kwa kufanya hivyo mahakama imepata fursa ya kutathmini uaminifu (credibility) wao?

    Lissu: Hayo ni ya majaji.

    Katuga: Ni kifungu gani cha sheria kinachoipa mahakama mamlaka ya kutowaamini polisi waliokuja kutoa ushahidi?

    Lissu: Utaratibu wa kuandika maelezo upo chini ya Kifungu cha 11(4) cha CPA. Kifungu hicho hakijaeleza chochote kuhusu hilo.

    Katuga: Umesema maelezo haya yalitakiwa yaandikwe mbele ya afisa wa polisi na si mpelelezi.

    Lissu: Ndiyo.

    Unaweza kusoma;

  17. Lissu akiri kuridhia yaliyomo kwenye vielelezo vyake mahakamani

    Katuga: Unakumbuka kwamba uliambia mahakama kuwa umetoa vielelezo D1 hadi D15. Je, ni vielelezo vyako au si vyako?

    Lissu: Ni vyangu kwa sababu mimi ndiye niliyeomba viingizwe mahakamani.

    Katuga: Je, nikisema kwamba uliomba vipokelewe mahakamani kama vielelezo vyako, umeridhika na yaliyomo ndani ya vielelezo hivyo?

    Lissu: Ndiyo, nimeridhika.

    Katuga: Umeridhika vitumike kama vielelezo vyako, na unaridhika na vielelezo ulivyovitoa?

    Lissu: Nimeridhika vitumike katika utetezi wangu.

    Katuga: Waheshimiwa Majaji, tunaomba vielelezo D1 hadi D15 ...

    Soma Zaidi Hapa:

  18. Uko timamu mzee wangu? Lissu aulizwa na upande wa serikali

    Katuga: Naona tutakaa hapa siku mbili

    Lissu: Unanitisha na siku mbili nimekaa ndani mwaka na miezi mitano

    Katuga: Iambie mahakama ulinzi wa mashahidi maana yake nini

    Lissu: Ni mashahidi wa kificho/ ni mashahidi wanaolindwa

    Katuga: Iambie mahakama, Je, ulisema baadhi ya watu huenda tulikuwa nao humu ndani. Je, huu ni ushahidi au hisia tupu?

    Lissu: Ndio ni shahidi wangu sababu hawajulikani hakuna anayewajua isipokua nyie

    Katuga: Je ushahidi wa kwamba hawa ni mapolisi. Je, ni ushahidi au fununu tu?

    Lissu: Ni ushahidi sababu hawajulikani na yeyote

    Katuga: Sasa shahidi tunataka majibu sahihi ni kweli au sio kweli. Ushahidi wa kwamba baadhi ya mashahdi huenda tulikuwa nao humu ndani. JE, ni kweli, sio kweli, sio wa kuona wala kusikia?

    Lissu: Sio Kweli

    Katuga: Iambie mahakama kama ni kweli au sio kweli unatuhuma nyingie za kuchapisha uongo mtandaoni

    Lissu: Ni kweli

    Katuga: Iambie mahakama unakumbuka ulisomewa hoja za awali na ikaanza kusikilizwa

    Lissu: Ndio nianakumbuka

    Katuga: Unakumbuka uliposomewa hoja za wali ulisema majaji ni ma-CCM

    Lissu: Sikumbuki

    Katuga: Iambie mahakama hii katika hotuba yako pia ulitangaza kutogumbea kwa chama chako

    Lissu: Sikumbuki, nakumbuka nilisema tutahamasisha ….

    Katuga: Hapana, hukumbuki nimsekia ukijiita mwenyekiti wa Chadema. Iambie mahakama kama chama chako kilishiriki uchaguzi mwaka jana

    Lissu: Hapana hakikushiriki

    Katuga: Je, ni kweli kwamba uliposema mahakamani hakuendeki huna imani na mahakama

    Lissu: Kwenye maswala haya ya uchaguzi sina imani na mahakama

    Katuga: Kwenye zile njia ulizotuambia jana. Je, nitakuwa sahihi kwamba hukupanga kabisa kuiomba mahakama kutumia sheria

    Lissu: Sikupanga kabisa

    Katuga: Kwa hiyo ni sahihi kwamba swala la kupinga sheria kwa njia ya mahakama sio njia mbadala wala ya kidemokrasia

    Lissu: Hapana

    Katuga: Kwa hiyo kukinukisha ni njia ya kidemokrasia?

    Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

    Katuga: Kuhamasisha uasi ni njia ya kidemokrasia?

    Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

    Katuga: Uko Timamu mzee wangu

    Lissu: Kimya

    Katuga: Kama nilikusia ulitamka vifungu vya 55, 63, 52 kifungu cha 52 cha sheria ya habari. Ni kweli kwamba sheria ya habari iliundwa kwa ajili ya kuendesha tasnia ya habari?

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kama nilikusikia vyema ulisema kuikosoa serikali sio kosa

    Lissu: Nilisema kuipinga serikali sio kosa

    Katuga: Kama una kanuni yako ya adhabu hapo kwa ridhaa ya mahakama hiki kifungu cha 55, yale maneno uliyotumbua, 'ya kuzuia uchaguzi' waambie majaji kuzuia uchaguzi ni kuipinga serikali au kuzuia uchaguzi?

    Lissu: NI kuzuia uchaguzi

    Katuga: Kuhamasisha uasi, kukinukisha nikupinga serikali au kupanga kuipindua serikali?

    Lissu: Ni kuipinga serikali, sikuwa nazungumza habari ya serikali tulikuwa tunapanga kuzuia uchaguzi

    Katuga: Unakumbuka umesema kwenye hotuba yako ulikuwa huzungumzii serikali

    Lissu: Ndio sikuwa napinga serikali nilikua nazungumza habari za uchaguzi

    Katuga: Kama nikikusikia vyema uliwaambia waheshimiwa hawa mashahidi wanaotoka jeshi la polisi, kasoro mmoja, wote wamejiandikia maelezo kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Waambie majaji kama uliwatajia kifungu cha sheria na sheria yenyewe

    Lissu: Sikuwaambia kifungu lakini kipo

    Katuga: Unajua kwamba askari aliyemuandika shahidi maelezo na yeye ni shahidi kama huyo shahdi hata fika mahakani

    Lissu: Sikumbuki

    Soma Zaidi Hapa:

  19. Lissu aendelea kujibu maswali ya upande wa serikali

    Katuga: Kama nilikusikia vyema uliiambia mahakama hii kwamba shahidi PW1 hakusema kama alivyogundua ni kosa la uhaini hakuwasiliana na ngazi za juu akiwemo DCI, kwamba ilipelelezwa vibaya

    Lissu: nilisema ilipelelezwa vibaya

    Katuga: Iambie mahakama kama sheria inaelekeza ukigundua kosa la uhaini lazima uwasiliane na hizo mamlaka zote, imabie mahakama kama ulitaja kifungu

    Lissu: Hapana sikutaja kifungu

    Katuga: Je unakumbuka ulisema kuna kutoelewana kati yako na Kingai (Kamishna wa Polisi Ramadhani Kingai ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini Tanzania) pamoja na IGP Wambura (Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Camillius Wambura)

    Lissu: Ni kweli nimekamatwa mara kadhaa bila kuzingatia taratibu

    Katuga: Umekuwa mwanasheria muda mrefu na mwana siasa miaka 24. Je, ushawafunguliwa wawili hawa mashitaka?

    Hapana: Sijawafungulia

    Katuga: Kama nimekusikia vizuri uliambia mahakama hii kwamba wale mashahdi walioletwa ni mashahidi ambao walikuwa ni washitakiwa

    Lissu: Nilisema walikiri kupanga uhalifu

    Katuga: Je, kuna sheria inayozuia mtu aliyefanya uhalifu kuja kutoa ushahidi?

    Lissu: Hapana

    Katuga: Katika ushahidi wa mashahidi toka Jeshi la polisi walieleza walikamata wote

    Lissu: Waliokamata waliweza kuwatambua

    Katuga: Kwa ushahidi huo ina maana inawezekana kukawa na wengine

    Lissu: Hawakutambuliwa au hawakukamatwa

    Katuga: Nakukumbusha ile kauli yako si ndio uliambia mahakama mtu yeyote anaweza kutafsiri vyovyote vile na wale walisema wamehamasika kutokana na nini

    Lissu: Maneno yangu

    Katuga: Kwa hiyo nitakuwa sahihi nikisema walielewa hotuba yako na kufanyia kazi maneno yako kwa jinsi walivyoelewa

    Lissu: Hapana siwezi sema sababu siwajui na siwezi kuwasemea

    Katuga: Je, uliiambia mahakama hawa mashahidi ni waongo na hawastahili kuaminiwa na mahakama?

    Lissu: Ndio, niliambia mahakama hawapaswi kuaminiwa wao na ushahidi wao

    Soma Zaidi Hapa:

  20. Upande wa serikali unaendelea na maswali ya dodoso kwa Tundu Lissu

    Wakili wa serikali (Nassoro Katuga): Umesema umepata tuzo kadhaa kwa kupigania haki. Je, ulitaja nchi za Afrika ulizopigania haki?

    Lissu: Hapana

    Katuga: Je uliiambia mahakama pamoja na kukaa kwako gerezani unasema heshima yako imeongezeka. Waambie majaji ni lini ulifanya huo utafiti ukajua heshima yako imeongezeka?

    Lissu; Heshima haitokani na sensa

    Katuga: Sasa wewe umejuaje heshima yako imeongezeka?

    Lissu: Heshima inaongezeka kwa watu kukuheshimu

    Katuga: Oooh pamoja na wazungu?

    Lissu: Hapana, sio wao tu, watu wote zikiwemo taasisi za kimataifa

    Katuga: Shahidi kama nilikuelewa vyema ukiwa unazungumzia mapungufu ya sheria za uchaguzi ulimuelezea mgombea wako wa jimbo la Mlimba kwamba alirudisha fomu akamkuta mtu hayupo. Ulikuwepo au uliambiwa?

    Lissu: Niliambiwa na nilisoma kweye taarifa rasmi

    Katuga: Waambie majaji kuwa mashahidi wa Jeshi la Polisi, hao mashahidi wa kificho hawajulikani na mtu mwingine

    Lissu: Ndio

    Katuga: Waambie waheshimiwa majaji kama uliwahi leta pingamizi juu ya kizimba cha mashahidi wa siri

    Lissu: Ndio

    Katuga: Iambie mahakama maamuzi ya mahakama ni nini

    Lissu" Waliamua wawaone wao

    Katuga" iambie mahakama hawa ulikua unawaIta P ni akina nani

    Lissu: Hayo ni majina, hizo ni alama, hayo ni mambo ya kuwaficha

    Katuga: Je unajua maamuzi ya mahakama hii juu ya kuficha utambulisho wa mashahidi

    Lissu: Iliamua wafichwe

    Katuga: Imabie mahakama ni sheria gani inayotaka ujue jina la shahidi ndio shahidi atoe ushahidi

    Lissu: CPA na Sheria ya Ushahidi inaelekeza mpaka ajulikane

    Katuga: Iambie mahakama

    Lissu: Kwa CPA na sheria ya mwenendo wa ushahidi, lazima afahamike na majaji na mahakama na watuhumiwa na sio upande wa utetezi peke yake

    Katuga: Waambie majaji ni kifungu gani cha CPA

    Lissu: Naomba nisome waheshimiwa majaji ni kifungu cha 112 kinachosema mashahidi watatoa ushahidi mbele ya hadhara ya mahakama na utambulisho wao utawekwa wazi, majina, dini zao na makazi yao

    Katuga: Je, kifungu kinasema hawatatoa ushahidi mpaka majina yao ya kweli yafhamike

    Lissu: Ndio hivyo kifungu kinasema

    Katuga: Waambie majaji wapi pameandikwa majina ya kweli yatajwe

    Lissu: Hakuna ila ni lazima mahakamma itambue utambulisho wao

    Katuga: Hivi unakumbuka wakati PW17 aliiambia mahakama baada ya kutoa hotuba, mliwatoa nje waandishi ili mkae kikao cha ndani

    Lissu: Ndio

    Katuga: Waambie majaji kama uliwahi kukanusha kama mliwatoa waandishi nje

    Lissu: Ndio hayakuwa yanawahusu tuliwaita kwa ajili ya mkutano na watia nia na sio zaidi ya hapo na baada ya kuwatoa waliondoka sio kwamba tuliwatoa na kuwarudisha

    Katuga: Unajua majibu yako yanavutia sana

    Lissu: Inabidi ufurahi kama yanavutia

    Katuga: Kwa hiyo nicheke cheke

    Lissu: Ndio cheka cheka si yanavutia sasa

    Katuga: Tafsiri sahihi inamaana wewe na wenzako mliwatoa waandishi wa habari

    Lissu: Ndio tuliwatoa

    Katuga: Mnasema mliwatoa sababu hayakua sehemu ya yale mliyowaitia

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kwa hiyo yale ambayo hamkutaka yachapishwe mliwatoa nje

    Lissu: Ndio

    Katuga: Kwahiyo unawaambia majaji yale yaliyochapishwa ni yale uliyotaka yachapishwe

    Lissu: Ndio yote tuliyotaka wawepo walikuepo waandishi wa habari na si vinginevyo, ila sikuwa lazimisha wachapishe

    Soma Zaidi Hapa: