Kielelezo kimepokelewa na kupewa jina D16
Lissu: Naomba apewe kielelezo D16.
Lissu: Umesema mlipopangiwa kazi na Boss wako John Marwa ukiwa pamoja na P1 sasa embu soma kwenye kielelezo chako.
Lissu: Tuendelee, umesema wazungumzaji wakuu kwenye mkutano huo walikuwa Lissu Heche na katibu mkuu hukumtaja jina ? embu angalia kielelezo kama kuna hayo maneno
Shahidi P: Upo wewe peke yako.
Lissu: Wala usiwe na wasiwasi nyie watu wangu hatugombani bwana hakuna katibu mkuu wala mnyika si kweli bwana P?
Lissu: Sasa shahidi leo umesema baada ya kupigiwa hiyo simu na boss wako ulikutana na afisa wa polisi uleyemkabidhi hiyo kadi na kuandika maelezo embu angalia maelezo yako kama hayo maneno yapo.
Shahidi P: Haya maelezo hayapo.
Lissu: Leo kwenye ushahidi wako umeulizwa siku hiyo ya mkutano ueleze muonekano wangu na ukajibu hivi alikuwa amevaa kombat ila rangi sikumbuki waeleze majaji kama yapo kwenye maelezo yako.
Lissu: Uliulizwa walikuwa wanarejelea uchaguzi wa serikali za mitaa kuelekea uchaguzi mkuu yapo hayo maneno hayapo?
Lissu: Umesema ulikuwa na wenzako mkiwa na kamera aina ya sonny NX kwemye maelezo yako mlikuwa na kamera tatu za sonny NX swali langu naomba uwathibitishie majaji kama ndio kamera yemyewe Sony HXA-MX100.
Shahidi P: Ndio ni kamera hiyo hiyo Nx ni kifupi.
Lissu: Naomba uthibitishe taarifa huo mkutano ulioelekezwa kuja ku cover alipata mwaliko toka kwa afisa habari wa Chadema.
Lissu: Waeleze majaji kama mimi ni afisa habari wa Chadema.
Lissu: Asante usiwe na wasiwasi unafanya kitu cha heshima unatoa ushahidi wa ukweli wa Mungu
Lissu: Waeleze majaji kama unafahamu afisa habari Chadema anaitwa Brenda Rupia.
Lissu: Kama nimekusikia sawa sasa umesema wewe na wenzako mlipofika HQ Chadema mlikuta wanachama wa chadema na watu wengine viongizi walikuwa hawajafika kweli sio kweli
Lissu: Waeleze majaji nani alikua anafanya maandalizi ya eneo la mkutano.
Shahidi P: Sikuzingatia hilo
Lissu: Waeleze majaji kama mimi nilikuwa sehemu ya wale waliokuwa wanafanya maandalizi kufuta vumbi na kukaribisha wageni.
Lissu: Mtu akikuambia huo mkutano aliyekualika ni Tundu Lissu na aliyefanya maandalizi ni Lissu atakua anasema ukweli au uongo?
Lissu: Sasa shahidi naomba uthibitisje kama ni kweli au sio kweli kina maneno yanayosema mlikua mnarusha matangazo yenu kwenye chaneli yenu ya Jambo na ikiwa yaliandikwa na wewe
Lissu: Naomba nikuhakishie pamoja na kwamba niko gerezani mwaka na zaidi hakuna mtu Chadema atakudhuru
Lissu: Kuna baadhi ya video tulizirusha kwenye mitandao ya x na youtube ambazo jambo ilirusha mtu akiingia atazikuta zipo?
Lissu: Bob Marley Alisema truth is never a sin
Lissu: Sasa shahidi nimeshitakiwa kwa uhaini na nimekua gerezani tangu ta rehe 10/04/2025 sababu inadaiwa mimi ndio nilirusha hizo video na kuweka kwenye mitandao ya Jambo TV waeleze majaji kama hii tuhuma ni ya kweli ni wewe na wenzako mlirusha au ni mimi.
Shahidi P: Sisi kupitia wewe.
Lissu: Nyie ndio mlirusha kupitia mimi.
Lissu: Waeleze majaji kama nilihusika na kamera zenu.
Lissu: Waeleze majaji kama niliwaelekeza kurusha hayo matangazo
Lissu: Je niliwaelekeza baada ya kurusha mbashara mchapishe kwenye mitandao ya kijamii?
Lissu: Ninaonewa tu sina hatia natuhumiwa kurusha tangazo
Shahidi P: Ni kweli wanakutuhumu lakini ndio maana tuko hapa mahakami ujitetee
Lissu: Ukisema ni kweli naenda kunyongwa hawa walioshitaki ndio wanachokitaka.
Lissu: Hebu naomba waeleze majaji kama ni kweli au sio kweli wewe ni shahidi uliyekueko kwenye mkutano huo.
Lissu: Shahidi katika kielelezo 16 kuna maneno yanasema hivi yakiyokua yanayoongelewa ni mambo ya uchaguzi na kauli mbiu ya no reforms no election na changamoto zao majimboni.
Lissu: Waeleze majaji kama viongozi wakiongea masuala ya uchaguzi na no reforms no election na matatizo ya majimboni kwao wanakuwa wamekosea
Lissu: Kuna maneno yafuatayo nataka uyathibitishe mimi nakumbuka matukio yote yaliyokua yakifanyika kwenye mkutano huo na yako kwenye memory kadi niliyokukabidhi, memory kadi uliyomkabidhi inspekta Chulu ni kweli sio kweli
Lissu: Video hizo hatujazifuta wala kuzihariri na mkutano ulifanyika kati ya saa mbili hadi tatu.
Lissu: hiyo memori kadi uliyomkabidhi inspekta Chulu hawajaleta mahakamani wala sijaona wala majaji au leo umeileta mahakamani?
Shahidi P: Hapana sijaleta
Lissu: Walileta kitu kingine majaji wakakikataa Kwenye maelezo yako shahidi hakuna uliposema maneno aliyozungumza Lissu ni makosa waeleze majaji kama ni kweli au sio kweli.
Lissu: Hakuna mahali umesema alichosema Lissu ni uhaini.
Lissu: Hakuna mahali umesema wewe na wenzako kwa kurusha mtandaoni mlikua mnasambaza uhaini.
Lissu: Ni kweli au sio kweli nyie waandishi wa Jambo hamkuwa peke yenu na walikuwepo waandishi wa vyombo vingine na vyote vilikua vinarusha hayo matangazo.
Shahidi P: Ni kweli walikuwa wanarekodi.
Lissu: Waeleze majaji kama vyombo vyote hivyo vilikuwa vinarekodi maneno ya kihaini.
Shahidi P: Sina hakika sababu mahakama haijathibitisha.
Lissu: Na kulikuwa na wasikilizaji viongozi wa chadema na watia nia na wote walisikia haya maneno.
Lissu: Ieleze mahakama kama wewe na wote waliokuepo mmeshtakiwa kwa kutotoa taarifa baada ya kusikia maneno hayo ya njama za kihaini
Lissu: Je, kuna mtu mwingine ameshitakiwa isipokua Lissu?
Lissu: Umesema mlikua Dodoma kikazi na mwenzako uliyemtaja kama P2 maelezo ya P2 anasema yeye ni mkazi wa Songea na hajawahi kwenda Dodoma kwenye hizo tarehe yeye akasema alikuwa Songea hiyo wewe unasemaje bwana?
Shahidi P: Ninachojua nilikua naye Dodoma
Lissu: Waheshimiwa majaji sina swali jingine ahsante shahdi
Shahidi anaruhusiwa kutoka. Upande wa jamuhuri hawana maswali ya Dodoso.
Jaji kama tumekubaliana kuwe na mashahidi wa kutosha tulete mashahidi.