Mliadhibiwa na mamlaka kwa kurusha mkutano wangu: Lissu
Mahojiano yanaendelea..
Wakili wa Serikali: Kwa namna unavyokumbuka yale maongezi walikuwa wanazungumzia uchaguzi gani?
Shahidi P: Serikali za mtaa kuelekea uchaguzi mkuu.
Wakili wa Serikali: Kwa shahidi huyu waheshimiwa majaji tunaomba tuishie hapa.
Lissu: Shahidi unanisikia bwana, hujambo?.. ninaomba nikuulize maswali kidogo na uyajibu kwa kweli ya Mungu.
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Iambie mahakama kuwa ninyi waandishi wa Jambo mmefanya kazi na mimi kwa muda mrefu sana.
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Na weleze majaji kama ni kweli au sio kweli mmekuwa mkitangaza mikutano yangu karibu nchi nzima.
Shahidi P: Kweli.
Lissu: Na waeleze waheshimiwa majaji mara nyingine nyie jambo TV ni chombo pekee kilichorusha mikutano yangu sehemu mbalimbali nchi hii.
Shahidi P: Kweli.
Lissu: Na waeleze majaji kama ni kweli au si kweli hata niliporudi nchini kutoka uhamishoni Ulaya ninyi waandishi wa habari wa Jambo TV mlinisindikiza nyumbani kwetu.
Shahidi P: Sikumbuki.
Lissu: Kuna Shedrack Simba na Oscar ni kweli si kweli.
Shahidi P: Ni kweli.
Lissu: Hawa nimekua nao katika kila mkutano niliokwenda nchi hii. Waeleze majaji hata siku ninakamatwa Mbinga, waandishi wa habari niliokuwa nao ni Shedrack Simba na Oscar ni kweli au sio kweli
Shahidi P: Ni kweli.
Lissu: Na waeleze majaji katika ziara zote hizo mkiwepo tumekuwa tukienda msafara mmoja na hata hoteli tunapofikia na tunakula pamoja ni kweli sio kweli ndugu yangu.
Shahidi P: Ni kweli
Lissu: Kama nitakuwa ninakosea waeleze majaji nyie watu wa Jambo na boss wenu tumekuwa na mahusiano ya karibu sana nitakuwa nakosea?
Shahidi P: Hapana hujakosea.
Lissu: Waeleze majaji kipindi chote ambacho tumefanya kazi pamoja mmekuwa marafiki zangu.
Shahidi P: Hujakosea.
Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji wakati mwingine vyombo vingine vikiogopa kurusha mikutano yangu nyie hamjawahi kuogopa kurusha mikutano yangu ni kweli sio kweli.
Shahidi P: Ni kweli.
Lissu: Iambie mahakama kuwa mliadhibiwa na mamlaka kwa kurusha mkutano wangu wa tarehe 3/4/2025
Shahidi P: Sikumbuki
Lissu: Hukumbuki mlifunguliwa kesi TCRA.
Shahidi P: Sikupata taarifa.
Lissu: Kwa mahusiano yetu mazuri nyie waandishi wa Jambo na boss wenu Marwa waambie majaji kama kuna mwanachadema amekutishia kukudhuru wewe au wafanyakazi wenzako wa jambo TV kwa namna yeyote ile.
Shahidi P: Hapana.
Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji tangu uliporusha mkutano mpaka leo kama kuna polisi yeyote au usalama uliyempa taarifa kama mnatishiwa wewe au wafanyakazi wenzako.
Shahidi P: Hapana sijafanya hivyo.
Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama una hofu yeyote kama una hofu ya kutoa ushahidi wako hadharani kila mtu akuone na akusikie
Shahidi P: Nina hofu kutoa ushahidi hadharani
Lissu: Unahofu gani bwana waeleze kwanini una hofu.
Shahidi P: Nina hofu sababu hili suala ni nyeti nyie ni viongozi nyie mnaweza msiwe na shida ila wafuasi wanaweza wasinielewe na wakanidhuru.
Lissu: Kama nimekuelewa vizuri sisi viongozi hatuna shida na hakuna mwanachama aliyekutishia.
Shahidi P: Ndio
Lissu: Uliandika maelezo Polisi?
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Waambie kama uliandikia maelezo Dodoma na aliyekuandika ni inspekta wa Polisi Andrew Chulu.
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Waheshimiwa majaji naomba nimsomee maelezo yake, naomba shahidi apewe nakala halisi ya maelezo yake ya Polisi.
Lissu: Shahidi umepata maelezo?
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Waeleze majaji sehemu ya makazi kama imefichwa.
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Na taarifa za mawasiliano binafsi simu barua pepe anuani?
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Na tarehe yako ya kuzaliwa?
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Na shule ulizosoma zimefichwa vilevile?
Shahidi P: Ndio
Lissu: Ulikwenda chuo cha kilimo vilevile imefichwa?
Shahidi P: Ndio.
Lissu: Nataka kuepuka uzembe wao hawa waliambiwa wafiche hawakuficha wanakiuka amri ya mahakama
Lissu anamsomea bila kusoma taarifa binafsi zitakazo fichua utambulisho wa shahidi licha ya kwamba karatasi aliyonayo ina taarifa zote za shahidi .
Lissu: Je unakubali maelezo yako haya yapokelewe kama kielelezo cha ushahidi mahakamani?
Shahidi P: Ndio.