Maswali ya dodoso kwa Lissu yakiendelea
Katuga: Kama nimekusikia vyema umesema ulitoa hotuba kwa watia nia wa Chadema na pia ulitoa hotuba hii mbele ya waandishi wa habari waambie majaji kama katika ushahdi wako umewaambia waandishi wa habaari wasipeleke rekodi zile na yale mliyozungumza.
Lissu: Hapana sikuwaambia.
Katuga: kwa hiyo ulitaka habari yako iende kwa walaji?
Lissu: Ndio nilitaka iwafikie wananchi.
Katuga: Katika ushahidi wako ulisema kama ulitoa mipaka kwa watu wanaopaswa kusikia ile hotuba.
Lissu: Hapana sikutoa mipaka
Katuga: Wale watia nia ulikua nao pale ambao ndio ulikuwa umewakusudia?
Lissu: Ndio walikuwepo
Katuga: Waambie majaji kama unakumbuka mkutano ulikuwa mubashara.
Lissu: Ndio ni kweli
Katuga: Waambie majaji kama uliwapa waandishi wa habari hotuba yako kabla kuzungumza.
Lissu: Hapana sikuwapa.
Katuga: Hivyo walikuwa hawajui unakwenda kuzungumza nini?
Lissu: Ni sahihi
Katuga: Kwa kuwa walikuwa hawajui nitakuwa sahihi nikisema haya maneno PW17 na wenzake walikuwa hawajui kabla ya wewe kuyatamka.
Lissu: Ndio walikuwa hawajui.
Katuga: Unakumbuka mashahidi walisema ulikuwa umevaa kombat na tishrt nyeusi?
Lissu: Ndio nakumbuka.
Katuga:Kuna sehemu umekanusha vazi ulilokuwa umevaa.
Lissu: Ningekanushaje vazi langu rasmi la chama?
Katuga: Kwa kuwa unasema ilikuwa hivyo nitasema mashahidi wa jamuhuri walikutambua kwa usahihi baada ya kutazama ile video.
Lissu: Ninasema mashahdi wa jamhuri wananitambua siku nyingi ni sahihi nilikua nimevaa hivyo.
Katuga: Unajua Principle ya constructive possession na constrtuction
Lissu: Hapana siijui.
Katuga: Umeiambia mahakama unakumbuka PW 17 alisema alichapisha kupitia wewe?
Lissu: Hapana alisema walichapisha wao kupitia Mimi. Waheshimiwa majaji naomba nikae hii mvua ya maswali inanielemea.
Jaji: Kaa.
Katuga: Unapotoa hotuba kila mtu si ana haki ya kuelewa na kutelekeza vile alivyoelewa?
Lissu: Ndio ni kweli
Katuga: Maneno ya kwamba tutazuia uchaguzi si kila mtu ana haki ya kuelewa alivyolewa?
Lissu: Ndio Maneno kama Tutazuia uchaguzi si kila mtu ana haki ya kuzuia uchaguzi kwa kutumia njia yake mwenyewe
Katuga: Unakumbuka PW3 alipotoa ushahidi na kusema walipanga kuzuia uchaguzi kwa kurusha mawe kuchoma moto baada ya kauli zako walipanga kurushia watu mawe wasiende kupiga kura iambie mahakama hii kwamba uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria.
Lissu: Ndio
Katuga: Mojawapo ya kazi za serikali ni kusimamia sheria
Lissu: Ndio
Katuga: Je, kuzuia watu kwenda kupiga kura kwa kuwarushia mawe ni uvunjifu wa amani sio ubunjifu wa amani?
Lissu: Ndio ni uvunjifu wa amani
Katuga: Na Jeshi la polisi liko chini ya nani?
Lissu: Jeshi la Polisi liko chini ya serikali
Katuga Unapotishia kuvunja amani umemlenga nani?
Lissu: Hapana unapovunja amani hujalenga polisi.
Katuga: Utanijibu tu ujanja hauna.
Lissu: Twende
Katuga: Anapotishia kuvunja amani anakuwa amefanyaje?
Lissu: Anakuwa analipa Jeshi la polisi kazi ya kumzuia asivunje amani.
Katuga: Kama niko sahihi ulisema unataka kuhamasisha maandamano ya kidemokrasia, je, kwenye haya maneno kuna maneno utahamasisha uasi wa kidemokrasia?
Lissu: Hapana
Katuga : Je, video ililetwa mahakamani au haikuletwa wewe si mkweli?
Lissu: Ililetwa ikakataliwa na mahakama.
Katuga: Je, wewe ungependa kuiona na kuiomba mahakama hii tukufu iilete mahakamani?
Lissu: Hapana hamuwezi mkaleta takataka nije niwasaidie mimi.
Katuga: Demokrasia inatoa haki kwa wote waounga mkono na wasio unga mkono yule anapenda kupiga kura. Je, yale maneno kuzuia uchaguzi yanatokana na demokrasia gani?
Lissu: Kama kuna jambo mnaona halipendezi mna haki ya kukipinga na kuliondoa kwa mujibu wa sheria.
Katuga: Je, unajua kuzuia uchaguzi ni kosa?
Lissu: Hapana sheria haijasema.
Katuga: Je, bado unasisitiza katiba inasema ni haki ya kikatiba kumzuia mtu kupiga kupiga kura kwa kufanya fujo?
Lissu: Katiba sio ibara moja.
Katuga: Tafsiri ya adhabu inaposema shall be liable pale ambapo kifungu cha sheria kinatoa maneno shall be liable je, kuna descretion ya mahakama?
Lissu: Hapana.
Katuga: Uko aware na kesi ya Shengi Muhagama?
Lissu: Niko Gerezani nitajuaje?
Katuga: Si ulikua unatoa kesi hapa?
Lissu: Wewe unaangalia mtandaoni hapo mimi naanngalia wapi?
Katuga: Si una watafiti we mzee?
Lissu: Waambie mmenishtaki kunyongwa kosa la bure.
Katuga: Unaweza kuisaidia mahakama tofauti ya mkanganyo na hapa halipo.
Lissu: Mkanganyiko ni kama jambo linalokuwa na maelezo mawili yanayotofautiana lakini omission ni jambo ambalo halipo lakini limechomekewa.
Katuga: umewahi kufungua shauri kwa jina lako kupinga sheria ya uchaguzi?
Lissu: Hapana, kwa chama changu Yes
Katuga: Kama nilikusikia vyema umeleta mambo ya jaji chande sana ya 29/10
Lissu: Ndio
Katuga: Je ni kweli kwamba ripoti yake ilisema pia matukio haya yalipangwa kabla kutokana na malalamiko ya muda mrefu ya mifumo ya uchaguzi, katiba ajira ……
Lissu: Nisomeee unikumbushe.
Katuga: Kwenye hotuba yako tuambie kama ulisema tukikinukisha watatufanya nini?
Lissu: Hapana.
Katuga: Sasa ulisema watanikamata watanifungulia kesi ya uhaini?
Lissu: Hapana.
Katuga: Unakumbuka kuwaambia majaji ni ma CCM?
Lissu :Ndio.
Katuga: Waheshimiwa majaji bado tuko nusu ila nikiangalia muda naona ni saa 11
Jaji: Mshtakiwa unasemaje?
Lissu: Waheshimiwa majaji kama ni saa 11 inatosha nimesimama ya kutosha kwa leo.
Jaji: Kimsingi tunatamani kuanza saa tatu kamili ili tuwe tumetumia muda vyema. Tutakapowahi tutaanza.
Tunahirisha mpaka kesho saa tatu asubuhi.