Nzengeli ahoji uhalali wa kampeni ya ‘No Reforms, No Election’
Nzengeli: Ni kweli kwamba wakati unafanya huo mkutano wa kuzuia uchaguzi hukuwa na kibali?
Lissu: Mikutano ya ndani haihitaji kibali, inahitaji taarifa tu.
Nzengeli: Hapo hukupi PGO?
Lissu: Ndiyo.
Nzengeli: Soma kifungu cha 40(3).
Lissu: 40(3), aya gani?
Nzengeli: Wakati natafuta, soma Sheria ya Vyama vya Siasa.
Lissu: Nisaidie kusoma ili tusipoteze muda.
Nzengeli: Soma kifungu cha 40(2), aya ya sita.
Lissu: (Anasoma.)
Nzengeli: Wewe umekielewaje?
Lissu: Nilichoelewa ni kwamba wakati wa mikutano ya kampeni, wanasiasa watatoa taarifa kwa polisi.
Nzengeli: Ni kweli au si kweli mkutano huo ulikuwa unazungumzia mambo ya uchaguzi?
Lissu: Haukuwa mkutano wa kampeni, na uchaguzi ulikuwa bado miezi sita mbele.
Nzengeli: Waheshimiwa majaji, ninaomba nimpe Sheria ya Vyama vya Siasa, kifungu cha 23.
Lissu: Nisomee.
Nzengeli: (Anasoma.)
Lissu: Ahsante, uliza swali.
Nzengeli: Je, kwa kifungu hiki ulipaswa kupeleka taarifa polisi?
Lissu: Hapana, si kweli, kwa sababu ulikuwa mkutano wa wazi na ulikuwa mkutano wa ndani.
Nzengeli: Shahidi, elewa swali.
Lissu: Mikutano ya ndani, dada yangu, haihitaji notification.
Lissu: Next.
Nzengeli: Ni kweli au si kweli huo mkutano unaouita wa ndani ulikuwa na waandishi wa habari?
Lissu: Ni kweli.
Nzengeli: Ambao ulikuwa mubashara na kila mtu aliuona?
Lissu: Ndiyo, ni mkutano wa ndani.
Nzengeli: Una kifungu chochote kinachokupa ruhusa ya kufanya mkutano wa ndani?
Lissu: Kifungu hicho hicho, kwa sababu hakuna mkutano unaohitaji ruhusa bali taarifa tu. Next.
Nzengeli: Wewe usinipangie.
Nzengeli: Je, maneno yaliyoko kwenye hati yako ya mashtaka unakiri uliyaongea?
Lissu: Nimesema sijatangaza maneno ya uhaini mbele ya waandishi wa habari.
Nzengeli: Uliyaongea au hukuyazungumza? Naomba uwaangalie majaji.
Lissu: Nimeshitakiwa kwa kuchapisha maneno yanayodaiwa kuwa ya uhaini kwa zaidi ya saa tatu.
Nzengeli: Uliyaongea au hukuyazungumza?
Lissu: Nimeongea kwa zaidi ya saa tatu.
Nzengeli: Je, ni kweli video ni kifaa tu kinachotumika kuchapisha?
Lissu: Hiyo inahitaji wataalamu.
Nzengeli: Kati yako na mahakama, nani anaweza kusema nani ni mhalifu?
Lissu: Mahakama ndiyo inaweza kusema mtu huyu ni mhalifu.
Nzengeli: Na ni kweli kwamba hujaleta namba za kesi za hao mashahidi wote ambao unasema ni wahalifu?
Lissu: Mapolisi si walifuta?
Nzengeli: Tuhuma ni shtaka au si shtaka?
Lissu: Tuhuma si shtaka.
Nzengeli: Shahidi, nimekusikia ukilalamika kuhusu mambo ya kukamatwa. Uliyapeleka hayo malalamiko mahakamani?
Lissu: Niliyapeleka na hakimu wa mahakama niliyemkabidhi alikataa. Ulitaka nifanyaje wakati niko gerezani?
Nzengeli: Unakubali kwamba sheria zote zilizotungwa na Bunge zinasimamiwa na Serikali?
Lissu: Sheria ya uchaguzi inasimamiwa na Tume ya Uchaguzi, si Serikali.
Nzengeli: Kwa hiyo sheria ya uchaguzi ni sheria kama sheria nyingine?
Lissu: Ni sheria.
Nzengeli: Ni kweli kwamba kuna tofauti kati ya kupinga uchaguzi na kuzuia uchaguzi?
Lissu: Waheshimiwa majaji, sisi tulitaka kupinga uchaguzi mpaka mabadiliko yafanyike. Shughuli zote za uchaguzi, majimbo yasitangazwe, wagombea wasitangazwe, kwa ujumla kila kitu kisimame.
Lissu: Utaratibu wetu wa saa kumi na moja umekuwa suspended.
Jaji: Ngoja tuulize, tulikuwa tunajua anamalizia.
Nzengeli: Kwa maelezo ya mshtakiwa, ni kweli amechoka na kibinadamu. Tunaomba tuahirishe.
Lissu: Kesho nayo ni siku.
Jaji: Tunaahirisha shauri mpaka kesho saa tatu asubuhi.