Moja kwa moja, Trump atangaza hatua kali zaidi za kiuchumi dhidi ya Iran na washirika wake

Shinikizo hili jipya la kulenga zaidi uchumi wa Iran linakuja wakati vita vya Iran vikielekea kutimiza miezi sita bila ya juhudi zozote madhubuti za kidiplomasia wala kijeshi.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi & Beldeen Waliaula

  1. Wanigeria 83 warejea nyumbani kwa kuhofia ghasia dhidi ya wahamiaji Afrika Kusini

    .

    Chanzo cha picha, EMMANUEL CROSET / AFP via Getty Images

    Kundi la raia 83 wa Nigeria limewasili mjini Lagos usiku wa Jumatano, huku kukiwa na wasiwasi unaoongezeka vurugu dhidi ya wahamiaji nchini Afrika Kusini.

    Watu hao walirejea nyumbani wakiandamana na maafisa wawili wa Ubalozi wa Nigeria jijini Johannesburg.

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria imrsema kuwa watu binafsi waligharamia usafiri wao, ikiongeza kuwa "zoezi la kurejesha nyumbani kundi hili la watu liliweezeshwa na wahisani wenye nia njema, ambao msaada wao uliwawezesha kuwarejesha salama nchini Nigeria."

    Mpango wa serikali wa kurejesha watu kwa hiari ulimalizika rasmi mwezi Julai.

    Waigeria 1,500 walirejeshwa nyumbani chini ya mpango huo.

    Serikali ilisema safari hizo ziligharamiwa kwa fedha za umma na kwamba watu hao hawakulazimika kulipia safari zao.

    Wanigeria wengine 66 walirejea mwezi Juni kwa safari tofauti ya ndege iliyoandaliwa na kugharamiwa na watu binafsi, kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje.

    Waliowasili hivi karibuni walipokelewa na Balozi Haruna Ali-Gombe, Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria.

    Kisha walikabidhiwa kwa taasisi husika za serikali kwa ajili ya taratibu za nyaraka na utambuzi kabla ya kuunganishwa tena na familia zao.

    Kurejea kwao kunakuja wakati Afrika Kusini inakabiliwa na maandamano mapya dhidi ya wahamiaji wasio na vibali halali.

    Baadhi ya makundi yametoa wito kwa wageni wasio na hadhi ya kisheria kuondoka nchini humo na yametoa makataa ya hadi Septemba 30 kwa wahamiaji wasio na vibali kuondoka.

    Afrika Kusini imeshuhudia maandamano kadhaa kuhusu uhamiaji mwaka huu, huku waandamanaji wakitaka kuwepo kwa udhibiti mkali zaidi.

    Serikali imelaani mashambulizi dhidi ya wahamiaji na kusema inaongeza juhudi za kutekeleza sheria za uhamiaji na kushughulikia uhamiaji usiofuata taratibu.

    Mamlaka za Afrika Kusini zinasema zaidi ya wahamiaji 80,000 wasio na vibali wamefurushwa nchini humo kama sehemu ya kampeni pana ya utekelezaji wa sheria.

    Serikali inasema itaendelea kuimarisha usalama wa mipakani na kutekeleza sheria za uhamiaji.

    Maelzo zaidi:

  2. Watu 13 wauawa Kyiv huku Ukraine ikikabiliwa na uhaba wa mifumo ya ulinzi wa anga

    '

    Chanzo cha picha, Reuters

    Takriban watu 13 wameuawa na wengine 34 kujeruhiwa katika mashambulizi ya hivipunde ya Urusi yaliyolenga mji mkuu wa Ukraine, huku Kyiv ikiendelea kukabiliwa na uhaba wa makombora ya ulinzi wa anga.

    Majengo ya makazi na maghala yalishambuliwa sehemu mbalimbali za jiji hilo usiku kucha, kulingana na Huduma ya Dharura ya Serikali ya Ukraine (DSNS), huku hospitali ya watoto na shule pia zikiharibiwa.

    Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kuwa ilitumia silaha za angani, nchi kavu na baharini kupiga vituo vya kijeshi na maghala, na kuongeza kuwa ndege zisizo na rubani 726 za Ukraine zilidunguliwa.

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema vifo hivyo vilitokana na uhaba wa makombora ya ulinzi wa anga, ambayo Kyiv hutegemea kupewa na washirika wake wa Magharibi.

    Akiandika kwenye mtandao wa Telegram, alisema "madamu Ukraine haina makombora ya kutosha ya kuzuia makombora ya balistiki, Urusi haitafikiria kwa uzito kuhusu amani".

    Mashambulizi hayo dhidi ya Kyiv yalianza majira ya saa sita usiku kwa saa za ndani huku ving'ora vya tahadhari ya mashambulizi ya anga vikilia jijini kote, yakifuatiwa na milipuko ya takriban makombora 20 ya Urusi.

    Mashambulizi hayo yalikatiza huduma za umeme katika maelfu ya majengo, na kuzitumbukiza baadhi ya sehemu za eneo la Kyiv gizani.

    Serikali imetangaza Ijumaa kuwa siku ya maombolezo kwa heshima ya watu waliouawa katika mashambulizi hayo.

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

  3. Deni la taifa la Marekani lavuka dola trilioni 40

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Takwimu kutoka Wizara ya Fedha ya Marekani zinaonyesha kuwa deni la taifa la Marekani limeongezeka maradufu ndani ya muongo mmoja, na kufikia dola trilioni 40.

    Ongezeko hilo linatokana na miaka kadhaa ya matumizi makubwa chini ya uongozi wa marais Donald Trump na Joe Biden, pamoja na kupanda kwa viwango vya riba ambavyo vimeendelea kuongeza jumla ya deni hilo.

    Mnamo mwaka wa 2016, deni la taifa la Marekani lilikuwa chini ya dola trilioni 20.

    Ofisi ya Bajeti ya Bunge ilikuwa imekadiria kuwa jumla ya deni hilo ingefikia dola trilioni 39.6 kufikia mwisho wa mwaka wa fedha wa 2026.

    Ongezeko hilo la kasi kuliko ilivyotarajiwa limezua wasiwasi kuhusu kasi ya ongezeko la mahitaji ya serikali ya Marekani ya kukopa fedha na athari zake kwa ongezeko la viwango vya riba hapo baadaye.

    Ofisi ya Bajeti ya Bunge inasema kuwa Marekani inakaribia dola trilioni 1.41 na inatarajiwa kufikia takriban dola trilioni 64 kufikia mwaka wa 2036.

    Wakati serikali ya Marekani ikitumia fedha zaidi kuziba pengo la bajeti yake, walaji wamejikuta wakikabiliwa na viwango vya juu vya riba na mfumuko wa bei.

    Soma zaidi:

  4. Mhadhiri wa Chuo Kikuu Tanzania adaiwa 'kutaka kuchoma majengo ya polisi'

    Melkisedek Kaijage

    Chanzo cha picha, Melkisedek Kaijage

    Wakili wa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kitunzi Kaijage anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi anasema mteja wake sasa anatuhumiwa kwamba alikuwa na nia ya kuchoma majengo ya umma pamoja na makazi ya askari Polisi katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania, ikiwemo Zanzibar.

    Akizungumza Agosti 19, 2026 jijini Dodoma, baada ya kesi dhidi ya mhadhiri huyo kuahirishwa, wakili Godfrey Wasonga alisema “Si majengo ya umma tu, pia anatuhumiwa kwamba anataka kuchoma makazi ya askari Polisi Tanzania nzima ikiwepo na Zanzibar”.

    Bw. Wesonga amesema tuhuma hizo zinahusisha majengo mbalimbali ya umma, ikiwemo shule, zahanati, mahakama na majengo mengine ya Serikali, huku akieleza kuwa suala hilo liko chini ya vifungu vya sheria ya kuzuia ugaidi.Wakili Wasonga amesema hatua inayofuata katika kesi hiyo ni uchunguzi wa awali, ambao unalenga kuwezesha shauri hilo kuwasilishwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa.

    Hata hivyo, kikao cha kesi hiyo kilichopangwa kufanyika Agosti 19 kiliahirishwa kwa sababu Hakimu Mkazi anayesikiliza shauri hilo, Zabibu Mpangule, hakuwepo.

    Kwa mujibu wa Wasonga, shauri hilo lilitajwa mbele ya Hakimu Kombe na sasa limepangwa kutajwa tena Agosti 27, 2026, ambapo pande zote zinatarajiwa kufahamisha mahakama hatua inayofuata.

    Wakili huyo amesema siku hiyo itatoa mwelekeo wa namna shauri hilo litakavyoendelea.

    Pia unaweza kusoma:

  5. Israel yatangaza zabuni ya mradi 'tata' wa makazi katika Ukingo wa Magharibi

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Israel imetangaza zabuni ya kujenga takriban nyumba 1,200 kwa ajili ya walowezi katika eneo lenye umuhimu wa kimkakati katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, huku ikijaribu kuondoa kabisa uwezekano wa kuwepo kwa taifa la Palestina.

    Mipango ya ujenzi katika eneo linalojulikana kama "E1" huko Jerusalem Mashariki imekuwa ikikosolewa vikali na jumuiya ya kimataifa kwa muda mrefu, na makazi hayo yanachukuliwa kuwa haramu kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

    Kupitia mpango huu, Ukingo wa Magharibi utagawanywa katika sehemu mbili, na Jerusalem Mashariki itatenganishwa na maeneo mengine.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, Ed Miliband, alikemea kutangazwa kwa zabuni hiyo akiitaja kuwa "kitendo kisichokubalika na kilicho na madhara" na kuitaka Israel "kusitisha mara moja mipango ya E1, kuondoa zabuni hiyo na kukomesha upanuzi wa makazi ya walowezi."

    Tangu Israel ilipokalia kwa mabavu Ukingo wa Magharibi na Jerusalem Mashariki wakati wa Vita vya Mashariki ya Kati vya mwaka 1967, imejenga takriban makazi 160, ambayo ni makazi ya Wayahudi wapatao 700,000.

    Wapalestina wanataka maeneo haya, pamoja na Ukanda wa Gaza, kwa ajili ya taifa lao la baadaye.

    Hivi sasa, takriban Wapalestina milioni 3.3 wanaishi sambamba na walowezi hao.

    Licha ya upinzani mkali kutoka kwa jumuiya ya kimataifa, serikali mfululizo za Israel zimeendelea kuruhusu upanuzi wa makazi hayo.

    Maelezo zaidi:

  6. Mkuu wa Ujasusi Ecuador, Wamarekani 5 wafariki ajali ya helikopta Kenya

    .

    Chanzo cha picha, Kenya Red Cross/Handout via Reuters

    Serikali ya Ecuador imesema mkuu wake wa Idara ya Ujasusi na mke wake wamefariki dunia katika ajali ya helikopta iliyoanguka jana Jumatano katika kaunti ya Samburu nchini Kenya.

    Raia watano wa Marekani pia walifariki dunia katika ajali hiyo, Msemaji wa Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani alisema.

    Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Kenya (KCAA) ilisema kuwa helikopta hiyo ilikuwa katika safari ya kutalii mandhari ikitoka kwenye hifadhi ya wanyamapori ya Loisaba kuelekea Ewaso Nyiro, mto unaopita kando ya hifadhi kadhaa za taifa.

    Kaunti ya Samburu ni mojawapo ya maeneo maarufu ya utalii nchini Kenya, ikiwa na hifadhi nyingi za wanyamapori zinazomilikiwa na sekta binafsi, na inajulikana kwa mandhari yake ya kuvutia na ya kipekee.

    Picha kutoka eneo la tukio zinaonesha moshi ukifuka katika eneo lenye miti ambapo helikopta hiyo ilianguka kwenye Mlima Ololokwe, huku wahudumu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya wakikaribia mabaki ya helikopta ambayo bado yalikuwa yakiteketea kwa moto.

    Ecuador haijatoa maelezo kuhusu kifo cha Sensi-Contugi, mwenye umri wa miaka 44, ambaye aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Ujasusi wa Kimkakati mwaka 2024.

  7. Jeshi la Israel lakiri kumuua msichana wa Kipalestina

    Hind Rajab

    Chanzo cha picha, Family/Reuters

    Maelezo ya picha, Hind Rajab, msichana wa Kipalestina wa umri wa miaka mitano aliyeuawa na jeshi la Israel

    Jeshi la Israel limethibitisha kwa mara ya kwanza kuwa wanajeshi wake walilifyatulia risasi gari alimokuwa Hind Rajab,msichana wa Kipalestina wa umri wa miaka mitano aliyeuawa pamoja na jamaa zake sita wakisafiri Gaza mnamo mwaka 2024.

    Gari la wagonjwa lililotumwa kumfikia—katika hatua iliyoratibiwa na jeshi la Israel—lilishambuliwa kwa makombora, na kusababisha vifo vya wahudumu wawili wa afya.

    Mwili wa Hind ulipatikana siku kadhaa baadaye, pamoja na miili ya watu wengine waliouawa.

    Katika taarifa, Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) limesema linaanzisha uchunguzi kuhusu vifo hivyo pamoja na mauaji ya wahudumu wawili wa afya waliotumwa kuokoa maisha ya Hind.

    Uchunguzi pia utaanzishwa kuhusu mauaji ya maafisa 15 wa kutoa misaada ya dharura waliouawa na wanajeshi wa Israel mjini Rafah mwaka jana.

    Matukio yote mawili yalilaaniwa kimataifa.

    Awali, Jeshi la Israel (IDF) lilisema kuwa hakuna hata mmoja wa askari wake aliyekuwa katika eneo hilo wakati Hind alipouawa. Hata hivyo, kauli hiyo ilianza kutiliwa shaka.

    Baadaye, IDF ilisema kuwa ilikuwa "imefanya operesheni dhidi ya maeneo yanayotumiwa na magaidi" kwa kutumia vikosi vilivyokuwa vikifanya kazi katika vitongoji vya Jiji la Gaza, ikiwemo Tel al-Hawa, ambapo Hind alikuwepo.

  8. Trump atangaza kuiwekea Iran vikwazo vikali vya kiuchumi

    Trump

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema anaanzisha vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya Iran na nchi yoyote ile itakayoisaidia au kufanya biashara nayo.

    Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social,Bwana Trump amesema anachukua hatua hiyo kwasababu Iran imeshindwa kufikia makubaliano na Marekani.

    Rais Trump ambaye mara kwa mara ametishia kuichukulia hatua kali zaidi Iran kwa kutoridhia kufikia makubaliano ya kuumaliza mzozo wa Mashariki ya Kati amesema leo anatangaza operesheni kali zaidi ya kiuchumi kuwahi kuchukuliwa dhidi ya nchi yoyote ile na itakuwa vita vya kiuchumi na kubaguliwa kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa.

    Aidha ametangaza kuwa nchi yoyote itakayoruhusu asasi zake za kifedha,biashara,viwanja vya ndege au asasi zake za kiserikali kuisadia kivyovyote vile Iran nayo itaathirika vibaya kiuchumi.

    Hata hivyo,hajatoa maelezo zaidi kuhusu hatua hizo mpya dhidi ya Iran au kutaja ni nchi zipi nyingine zitakazolengwa na vikwazo hivyo vipya.

    Kauli ya Trump inakuja wiki moja baada ya waziri wake wa fedha Scott Bessent kusema Marekani itaiwekea vikwazo vya kiuchumi Iran kwa viwango ambavyo havijashuhudiwa katika kipindi cha nyuma.

    Makubaliano ya kusitisha vita vya Iran kwa siku sitini yalikamalika Jumatatu wiki hii huku kukiwa hakuna dalili za kukomeshwa kwa mzozo huo wa Mashariki ya Kati.

    Shinikizo hilo jipya la kuulenga zaidi uchumi wa Iran linakuja wakati vita vya Iran vikielekea kutimiza miezi sita bila ya juhudi zozote madhubuti za kidiplomasia wala kijeshi.

    Rais Trump aliyevianzisha vita hivyo mwishoni mwa mwezi Februari pamoja na Israel, anamulikwa darubini kali kisiasa nchini mwake wakati nchi hiyo ikijiandaa kwa uchaguzi wa katikati mwa muhula unaotarajiwa mwezi Novemba.

    Mshirika wake katika vita hivyo vya Iran,Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu naye anakabiliwa na shinikizo la kisiasa kuhusu anavyoshughulikia mzozo wa Iran na wa Gaza kuelekea uchaguzi mkuu wa Israel unaotarajiwa mwezi Oktoba mwaka huu.

    Licha ya mashambulizi ya makombora kupungua katika siku za hivi karibuni kati ya Iran na Marekani,Iran imeendelea kuzuia meli kupita katika Mlango Bahari wa Hormuz licha ya shinikizo kali kutoka kwa Marekani kutaka njia hiyo muhimu ya safari za meli za mizigo baharini kufunguliwa.

    Soma zaidi:

  9. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja leo Alhamisi 20.08.2026.