Iran: Hakuna hatua iliyopigwa kufufua makubaliano ya muda ya amani na Marekani

Chanzo hicho kimesema hakuna hatua iliyofikiwa katika mazungumzo ya kufufua makubaliano ya muda ya mwezi Juni.

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid, Asha Juma na Sarafina Robi

  1. Caroline Levitt kujiuzulu kama msemaji wa Ikulu ya Marekani - Trump

    x

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Caroline Levitt, atajiuzulu wadhifa huo mwishoni mwa mwezi huu.

    Trump amesema katika ujumbe kwenye mitandao ya kijamii kwamba Levitt anaondoka kwenye nafasi hiyo ili kutumia muda zaidi na watoto wake wadogo pamoja na familia yake, akisema kuwa anaelewa na kuheshimu uamuzi huo kikamilifu.

    Trump amemtaja Caroline Levitt kuwa miongoni mwa wasaidizi wake anaowaamini zaidi.

    Rais huyo ameongeza kuwa Levitt sasa atakuwa mmoja wa washauri wake muhimu wa nje ya serikali na ataendelea kuwa sauti yenye ushawishi ndani ya Chama cha Republican.

    Levitt, mwenye umri wa miaka 28, aliteuliwa kuwa msemaji wa Ikulu mwaka jana na kuwa mtu mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kushika wadhifa huo.

    Hadi sasa haijafahamika mara moja ni nani atakayemrithi katika nafasi hiyo.

  2. Serikali ya Uingereza yaonya kuhusu athari za kufungwa kwa Mlango wa Hormuz kwa uchumi

    x

    Chanzo cha picha, AP

    Serikali ya Uingereza imeingiwa na wasiwasi kwamba kuendelea kwa usumbufu wa usafirishaji wa meli kupitia Mlango wa Hormuz kunaweza kudhoofisha zaidi ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo mwakani.

    Makadirio ya ndani ya Hazina ya Uingereza yanaonyesha kuwa iwapo usumbufu huo utaendelea hadi mwisho wa mwaka, ukuaji wa Pato la Taifa unaweza kushuka hadi asilimia 0.3 mwaka 2027.

    Maafisa wa Hazina wamewasilisha tathmini hiyo kwa Waziri Mkuu, huku serikali ikisema inaendelea kujiandaa kwa matukio mbalimbali yanayoweza kujitokeza.

    Hata hivyo, serikali imeonya kuwa makadirio ya ukuaji wa asilimia 0.3 yanatokana na hali mbaya zaidi kuliko ilivyotarajiwa, na si utabiri wake wa msingi.

    Tathmini hiyo inakuja wakati uchumi wa Uingereza tayari ukikabiliwa na ukuaji dhaifu. Maafisa wanatarajiwa kufuatilia kwa karibu takwimu mpya za Pato la Taifa ili kubaini athari za mzozo huo kwa uchumi.

    Vita vya Mashariki ya Kati na mzozo kati ya Marekani na Iran vimesababisha kupanda kwa bei za nishati na kuvuruga kwa kiasi kikubwa usafirishaji wa meli kupitia Mlango wa Hormuz, njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani.

    Soma Zaidi:

  3. Marekani na Iran zatoa madai kinzani kuhusu udhibiti wa Mlango wa Hormuz

    D

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump amesisitiza tena kuwa Marekani ina “udhibiti kamili” wa Mlango wa Hormuz, licha ya kupungua kwa shughuli za usafirishaji katika njia hiyo muhimu ya majini hadi kiwango cha chini zaidi kwa wiki moja, huku vita dhidi ya Iran vikiendelea.

    Kwa upande wake, Tehran imesisitiza msimamo wake wa kuendelea kupinga Marekani na kuufanya Mlango wa Hormuz ubaki umefungwa hadi masharti yake yote yatimizwe.

    Trump amesema watu wengi wanaita kizuizi cha Marekani katika Mlango wa Hormuz “ukuta wa chuma” na kwamba Iran haina uwezo wa kukizuia.

    Katika ujumbe kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, Trump amesema Marekani ina udhibiti kamili wa Mlango wa Hormuz na kuongeza kuwa anaamini itaendelea kuudhibiti.

    Trump amedai Iran haina jeshi la wanamaji wala jeshi la anga, huku wanajeshi wa Iran wakidaiwa kutolipwa mishahara. Pia amesema Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC, limedhoofishwa pakubwa na linarudi nyuma.

    Aidha, Trump amesema hali ya uongozi wa Iran bado haijulikani, huku akidai nchi hiyo haina fedha na kwamba kinachobaki ni “habari za uongo na mfumuko wa bei wa asilimia 300”.

    Trump amesisitiza kuwa Iran huzungumza tu bila kuchukua hatua.

    Unaweza kusoma;

  4. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja ya tarehe 13/08/2026.