Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Iran yaweka masharti kabla ya kufungua tena Mlango Bahari wa Hormuz

Marekani, kwa upande wake, inaendelea kusisitiza kuwa Mlango wa Hormuz uko wazi na kwamba mabomu ya baharini yameondolewa, huku ikisema hakuna mazungumzo yaliyopangwa kwa sasa na Iran.

Muhtasari

Iran yaweka masharti kabla ya kufungua tena Mlango Bahari wa Hormuz

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. Idadi ya watu waliofariki Nepal na Tibet yafikia 469 huku kukiwa na hofu ya mafuriko zaidi

    Takriban watu 469 wamefariki dunia nchini Nepal na mamia hawajulikani walipo baada ya mafuriko makubwa ya ghafla yaliyokumba eneo la milimani mpakani mwa Nepal na Tibet Jumatano.

    Nchini Tibet, watu watatu wamefariki na zaidi ya 550 hawajulikani walipo. Haijafahamika iwapo baadhi ya watu hao wamehesabiwa pia katika takwimu za Nepal.

    Waokoaji wanaendelea kuwasaka manusura, lakini wanakabiliwa na hofu ya kutokea kwa mafuriko mengine katika eneo lililoharibiwa.

    Shirika la Msalaba Mwekundu limeiambia BBC kuwa waokoaji wako katika hali ya tahadhari kutokana na ripoti kwamba wimbi jingine la mafuriko linaweza kulikumba eneo hilo.

    Ziwa lenye maji yanayoongezeka limejitokeza karibu na mpaka wa China na Nepal, hali inayozua hofu kwamba huenda kingo zake zikapasuka na kusababisha mafuriko mengine.

    Maafisa wa eneo hilo wameiambia BBC kuwa kuporomoka kwa barafu ya mlima kulisababisha wimbi kubwa la maji lililosomba nyumba na barabara, pamoja na kuharibu kituo muhimu cha mpakani kinachounganisha Nepal na Tibet.

    Eneo hilo hutembelewa na makumi ya maelfu ya watalii kila mwaka.

    BBC imezungumza na ndugu za baadhi ya watu ambao bado hawajulikani walipo.

    Dada wawili ambao wazazi wao hawajulikani walipo wameeleza matumaini yao ya kuwaona tena, wakisema: "Tunawapenda sana na tunataka warudi nyumbani."

    Soma Zaidi hapa:

  2. Iran yaweka masharti kabla ya kufungua tena Mlango Bahari wa Hormuz

    Mkuu wa usalama wa Iran, Mohsen Rezaei, amesema Tehran inaandaa orodha ya masharti ambayo Marekani inapaswa kutimiza kabla ya Iran kuruhusu tena usafirishaji kupitia Mlango wa Bahari wa Hormuz.

    Amesema hatua hiyo imekuja kufuatia maombi kutoka kwa wapatanishi wanaojaribu kupunguza mvutano kati ya Iran na Marekani.

    Katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Qatar, Sheikh Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema utawala wa Rais Donald Trump unafanya maamuzi yasiyo sahihi kwa kutegemea taarifa potofu.

    Ghalibaf amesema Washington lazima itekeleze ahadi zake chini ya MOU kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.

    Waziri Mkuu wa Qatar yuko Tehran katika juhudi za upatanishi, huku akijadili pamoja na viongozi wa Iran masuala muhimu, likiwemo suala la Mlango wa Hormuz na uwezekano wa kuanza tena kwa mazungumzo kati ya Tehran na Washington.

    Marekani, hata hivyo, inaendelea kusisitiza kuwa Mlango wa Hormuz uko wazi na kwamba mabomu ya baharini yameondolewa, huku ikisema hakuna mazungumzo yaliyopangwa kwa sasa na Iran.

    Soma Zaidi Hapa:

  3. Hujambo, natumai umzima na karibu kwa matangazo yetu ya moja kwa moja ya leo Ijumaa.