Marekani na UN zatoa msaada kwa waathiriwa wa mafuriko Nepal

Chanzo cha picha, EPA
Marekani imeahidi kutoa msaada wa dola 500,000 ambazo zitatumika kugharamikia makazi ya muda, maji, huduma za usafi na misaada mingine kwa jamii zilizoathiriwa na mafuriko.
“Marekani inatuma salamu zake za rambirambi kwa familia na jamaa wa waliofariki katika mafuriko makubwa ya ghafla yaliyoikumba wilaya ya Rasuwa nchini Nepal,” Idara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani ilisema katika taarifa.
Takriban raia 54 wa Marekani, wengi wao wakiwa watalii, wameripotiwa kuwa miongoni mwa mamia ya watu waliopotea kufuatia mafuriko na maporomoko ya ardhi.
Hayo yakijiri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema “amehuzunishwa na mafuriko hayo makubwa” ambayo yamesababisha vifo vya watu wengi, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo nchini Nepal na China.
“Nasimama pamoja na wote walioathiriwa,” amesema kiongozi huyo.
Ameongezea kuwa timu za Umoja wa Mataifa na washirika wake zinaandaa kusafirisha vifaa pamoja na kuwapeleka wahudumu wa dharura nchini Nepal ili kuisadia kukabiliana na janga hilo.
Soma pia:



